Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (katikati), akiwaasa wafanyabiashara wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma (hawapo pichani) kutumia fursa zilizopo katika nchi jirani ikiwemo Burundi kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani ili kukuza uchumi wa Wilaya hiyo, alipofanya mkutano na Wafanyabiashara hao Wilayani hapo, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala, na kulia ni Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Kakonko Bw. Kadudusi Bunabuna.
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, Kanali Hosea Ndagala, akiwataka wafanyabiashara wa Wilaya hiyo kuzingatia taratibu za kibiashara na kuhakikisha wanajipanga kuanzisha viwanda vidogo ili kuongeza thamani ya bidhaa wanazouza nje ya nchi, wakati wa mkutano kati ya Wafanyabiashara wa Wilaya hiyo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (wa pili kushoto).
Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA anaye shughulikia mapato ya ndani Bw. Elijah Mwandumbya, akifafanua masuala mbalimbali ya kikodi kwa wafanyabiashara wa wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma, wakati Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji alipokutana na wafanyabiashara hao kujadili fursa na changamoto wanazopata.
Wafanyabiashara Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma wakimsikiliza kwa Makini Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (hayupo pichani), alipofanya mkutano ulioangazia namna bora ya kuboresha mazingira ya kibiashara katika Wilaya hiyo.
Maafisa wa Wizara ya Fedha na Mipango walioko kwenye msafara wa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, wakifuatilia mkutano kati ya Serikali na wafanyabiashara wa wilaa ya Kakonko mkoani Kigoma.
Mfanyabiashara wa Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma Bw. Musa Ndiliwe, akieleza kuhusu kuimarishwa kwa mazingira bora ya kibiashara katika Soko la Ujirani mwema kati ya yao na wenzao wa Nchini Burundi kwa lengo la kukuza biashara, wakati wa mkutano kati ya wafanyabiashara hao na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) Wilayani hapo.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)
Na.Benny Mwaipaja, Kakonko, Kigoma
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji,
amewashauri wakazi wa Wilaya ya Kakongo na mkoa wa
Kigoma kwa ujumla kuchangamkia fursa za biashara kati ya
mkoa huo na nchi jirani za Rwanda na Burundi kwa kuuza
mazao ya kilimo yaliyochakatwa likiwemo zao la muhogo ili
waweze kunufaika na biashara hiyo ya mipakani.
Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo mjini Kakonko baada ya kukutana
na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa wilaya
hiyo,mkutano uliolenga kujadili fursa na changamoto za
ufanyaji biashara katika eneo hilo yakiwemo masuala ya
kikodi.
"Nakuomba Mkuu wa Wialaya ya Kakonko uwakutanishe na
kuwaunganisha wafanyabiashara hawa ambao nafurahi
wengi wao ni vijana ili waandae andiko la namna ya
kununua mashine za kuongeza thamani ya mazao ili wauze
nje yakiwa yamechakatwa badala ya mfumo wa sasa ambao
wanauza mazao ghafi nje ya nchi na hivyo kupata hasara"
alisisitiza Dkt. Kijaji
Awali, wafanyabiashara wa Kakonko walimweleza Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu kijaji,
aliyeambatana na Kamishna wa Mapato ya ndani wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. Elijah
Mwandumbya, kwamba, bei ya zao la muhogo imeshuka
kutoka shilingi 600 kwa kilo katika msimu uliopita hadi
kufikia shilingi 150, hali iliyowasababishia wakulima
maumivu makubwa.
"Wafanyabiashara wanaonunua mazao yetu kutoka Burundi
ni watu wa kati kwa maana ya madalali ambao wananunua
mazao yetu kwa bei nafuu na kuyapeleka n hini kwao ambako
huyachakata na kuyauza kwa bei kubwa nchini mwao na
nchi za Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo,
hivyo tunaiomba Serikali itupatie mikopo kupitia Benki ys
Kilimo ili tusnzishe viwanda vya kuchakata mazao yetu"
alieleza mfanya biashara Dkt. Brighton Gwamagobe
Akizungumza katika Mkutano huo, Kamishna wa TRA wa
Mapato ya Ndani Bw. Elijah Mwandumbya, pamoja na kutoa
ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kodi, ametoa wito kwa
wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari ili kuiwezesha
Serikali kupata fedha za kuhudumia jamii ikiwemo ujenzi wa
miundombinu ya barabara, afya, maji na mambo mengine
kadha wa kadha.
Alisema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya
ukusanyaji kodi na kutatua kero mbalimbali za
wafanyabishara pamoja na kuongeza wigo wa walipa kodi ili
kuimarisha mapato ya nchi
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, yuko
katika ziara ya kikazi mkoani Kigoma ambapo anakagua
miradi mbalimbali ya maendeleo inayopatiwa fedha na
Serikali pamoja na kuzungumza na jumuiya ya
wafanyabiashara.
No comments:
Post a Comment