Habari za Punde

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Ndg.Dotto James Akabidhi Matrekta 10 Kwa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo SUA Katika Kiwanda Cha URSUS-TAMCO Kibaha Mkoani Pwani.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Profesa Raphael Chibunda wapili kutoka (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa NDC Profesa Damian Gabagambi wakwanza (kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo wapili kutoka (kulia), akikata utepe kuzindua Matrekta 10 ambayo ameyakabidhi kwa Chuo hicho cha SUA kutekeleza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akipunga mkono pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuzindua na kuyakabidhi Matrekta hayo 10 kwa Chuo cha SUA katika hafla fupi iliyofanyika katika kiwanda cha kuunganisha Matrekta hayo cha URSUS- TAMCO Kibaha mkoani Pwani.

Sehemu ya Matrekta 10 yaliyokabidhiwa leo kwa Chuo cha SUA ikiwa ni  utekelezwaji wa  ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.