Habari za Punde

Ligi ya Premia: Njia tano za kuwazuia Manchester City msimu wa 2018-19

Kikosi cha Pep Guardiola kinaonekana kuwa kitashinda msimu ligi kuu ya England msimu wa 2018-19.
Klabu kumi na tisa zilijaribu kuizuia Manchester City kushinda mechi Ligi kuu ya England msimu uliopita. Sita tu zilifaninkiwa.
Mwaka 2017-2018 City walipata pointi nyingi zaidi kuliko timu yoyote ile na kuandikisha ushindi mara nyingi na kufunga mabao mengi kuliko timu yoyote katika ligi kuu ya England iliyowatangulia.
Katika maandalizi ya msimu wa 2018-19 mabingwa hao walitumia pauni milioni 70 kumsaini mchezaji bora wa Ligi mwaka ya 2015-16 Riyad Mahrez.
Hizi ni mbinu ambazo timu zote 19 zinazoweza kutumiwa na timu 19 kuikabili Manchester City.
City wanajua kudhibiti mpira uwanjani na wana kasi ya juu, ni rahisi kuvutiwa na mchezo wao lakini ni vigumu kucheza kama wao.
Lakini wachezaji waliopangwa vizuri wanaweza kuleta matokeo mazuri jinsi Liverpool walivyoonyesha wakati kikosi cha Guardiola kilipata pigo mikononi mwao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.