Habari za Punde

Shirika la Mawasliani Nchini TTCL Waahidi Kuongeza Gawio Zaid Mwaka 2019.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (mwenye suti nyeusi) hivi karibuni akiongea na Kamati ya maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane alipotembelea banda la Mamlaka kwenye Uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba (kulia) akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Afisa Mipango na Takwimu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Edward Kimaro alipotembelea banda la Maonesho ya Kilimo na sherehe za Nanenane la Mamlaka, yanafanyika kwenye Uwanja wa Nyakabidni mkoani Simiyu.

Baadhi ya wanakamati ya maonesho ya Kilimo na sherehe za Nanenane ya Mamlaka ya Viwanja wa Ndege Tanzania (TAA), wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) (mwenye suti).

Afisa Biashara na Masoko wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Herieth Nyalusi (kulia) akitoa maelezo ya ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege cha Mkoa wa Simiyu kwa Bi. Grace Kenedy (kulia) na Bi.Magreth Lend wakazi wa Bariadi, walipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa Nyakabindi.

Raia wa China wanaofundisha kwenye shule ya ya sekondari ya J.W.Bukanga Musoma, Bi. Jane Lee (wapili kushoto) na  Bi. Cary Zhang (watatu kushoto) wakimsikiliza Afisa Usalama Mwandamizi wa Mamlaka wa Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Bakari Mwalwisi alipokuwa akitoa maelezo kuhusu vimiminika kwenye banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane la Mamlaka yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi, mkoani Simiyu. 


Na Mwandishi Wetu, Simiyu

SHIRIKA la Mawasiliano nchini (TTCL), limeahidi kutoa 

gawio kubwa zaidi kwa serikali mwakani, ili fedha hizo 

zikasaidie katika kazi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa 

miundombinu ya viwanja vya ndege vya serikali.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri 

Kindamba ambaye alitembelea banda la maonesho ya Kilimo 

la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), 

yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi mkoani 

Simiyu, amesema wingi huo wa fedha utatokana na 

mashirika na taasisi za umma kuwaunga mkono kwa 

kutumia huduma mbalimbali zinazotolewa na shirika hilo.

“Mwaka huu tulitoa gawio la sh. Bil 5.1 kwa serikali, lakini 

ninaimani mwakani tutatoa zaidi endapo tutapata 

ushirikiano wa kutumiwa kwa huduma zetu kutoka kwenye 

taasisi nyingine za serikali, ambapo fedha 

hizo zinasambazwa na serikali kwenye kazi mbalimbali 

ukiwemo wa ujenzi wa viwanja vya ndege,” amesema Bw. 

Kindamba.

Bw. Kindamba ameishukuru TAA kwa kuanza kutumia 

huduma ya mawasiliano ya simu kutoka kwenye shirika hilo, 

ambapo itasaidia kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi. 

Amesema anaahidi kuimarisha ushirikiano na TAA, na wapo 

tayari kutumia huduma zinazotolewa na mamlaka kwa 

maslahi ya nchini, ili kuimarisha na kukuza uchumi wa nchi.

“Ushirikiano wetu utasaidia kuongeza mapato, ambapo kila 

taasisi moja itaweza kutumia huduma na bidhaa za taasisi 

nyingine, kwa lengo la kuzifanya ziendelee kukua na 

kuimarika kiuchumi, kwani taasisi za umma zinategemeana 

zenyewe kwa zenyewe,” amesema.

Pia ameipongeza TAA kwa jitihada zake za kujitangaza kwa 

wananchi, ambapo ameitaka kuendelea kuboresha 

miundombinu ya viwanja vya ndege.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kujitangaza, 

naomba muendelee kuboresha viwanja vya ndege kwa 

maslahi ya Watanzania wote, kwa kweli najivunia sana 

uwepo wenu katika Nanenane “I am proud of your success’ 

na kweli mna iunganisha Tanzania kwa Ulimwengu,” 

amesema Bw. Kindamba.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.