Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akiwa amesimama pemebezoni
mwa Mto Mara eneo la ‘Kogatendo’ na kupata maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa
Serengeti Bw. William Mwakilema juu ya kupungua kwa maji katika Mto huo. Waziri
Makamba ameahidi kuipatia ufumbuzi changamoto hiyo mapema iwezekanavyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akiwa amesimama pemebezoni
mwa Mto Mara eneo la ‘Kogatendo’ na kupata maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa
Serengeti Bw. William Mwakilema juu ya kupungua kwa maji katika Mto huo. Waziri
Makamba ameahidi kuipatia ufumbuzi changamoto hiyo mapema iwezekanavyo.
Bw. William Mwakilema
(kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba mara
baada ya kutembelea Mto Mara eneo maalumu ambalo wanyama aina ya nyumbu huvuka
kwa makundi na kuwa kivutio kikubwa cha utalii.
Eneo la Kogatendo katika
Mto Mara ni miongoni mwa maeneo ambayo wanyama aina ya nyumbu huvuka kwa
makundi na kuwa kivutio cha utalii. Waziri mwenye dhamana ya usimamizi wa
Mazingira January Makamba ametembelea eneo hilo ili kuhakikisha hatua
zinachukuliwa kurejesha ikolojia ya mto huo katika hali ya awali.
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Mhe. January Makamba amewakumbusha
watendaji wa Wilaya ya Serengeti wajibu wao wa kipekee wa
ulinzi katika hifadhi
ya mbuga ya Serengeti kwakuwa Wilaya
yao imebeba jina linalojulikana duniani kote
ikiwa ni pamoja
na eneo maalumu la wanyama aina ya Nyumbu ambao
huvuka kwenda
upande wa pili na kuwa miongoni mwa
vivutio vikubwa vya utalii.
Waziri Makamba ameyasema
hayo leo Wilayani Serengeti
mara baada ya kufanya ziara ya kikazi Wilayani hapo
kujionea uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira na kutembelea
eneo la mto Mara eneo
ambalo ni muhimu sana ki-ikolojia.
Katika kikao na viongozi
wa Wilaya hiyo, Mhifadhi Mkuu wa
Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Bw. Wiliam
Mwakilema
aliainisha kuwa mtiririko wa maji katika Mto Mara kutoka
chanzo chake
kikuu katika Milima ya Mau nchini Kenya
kimepungua kutokana na shughuli za
kibinadamu na
matumizi mengine yasiyoendelevu jambo linalohatarisha
kupungua
kwa mtiririko wa maji katika Mto Mara kwa
kipindi kirefu, eneo ambalo ni kivutio
pekee cha wanyama
wanaohama dunia.
Katika kutatua tatizo hilo
Waziri Makamba amesema kuwa
masuala ya mazingira ni mtambuka hivyo Ofisi yake
yenye
dhamana na kusimamia hifadhi ya Mazingira nchini itafanya
ziara ya kikazi
nchini Kenya kwa lengo la kujadiliana na
kupata ufumbuzi wa haraka juu ya jambo
hilo.
“Sisi na wenzetu wa Kenya
tumeingia mkataba mwaka 2013
wa matumizi sahihi ya rasilimali katika Mto Mara
na kutunza ikolojia yake, kwa kushirikiana na Mawaziri wenzangu wa Maji na
Maliasili na Utalii, tutafanya ziara nchini Kenya ili kwapamoja tupate ufumbuzi
wa jambo hili ikiwa ni pamoja na Ziwa Chala, Ziwa Jipe na Ziwa Natroni ambayo
yote yako pande mbili yaani Tanzania na Kenya.”
Waziri Makamba amesema
Serikali itahakikisha maslahi ya
Nchi yanalindwa kwa njia za ki-diplomasia na
kuhakikisha
Mto Mara unatiririsha maji kipindi chote cha mwaka.
Waziri Makamba amehitisha
ziara yake Mkoani Mara na
amewasili Mkoani Arusha ambapo atakuwa na vikao wa
wadau wa hoteli mbalimbali na kambi za uwindaji kwa lengo
la kuweka mikakati ya
kuhifadhi mazingira maeneo ya
mbugani.
No comments:
Post a Comment