Mwakilishi wa Waganga wa Tiba Asili Zanzibar akisoma Risala ya Jumuiya yao Wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Tiba Asilia Barani Afrika.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi: Waziri Biashara Viwanda na Masoko
Zanzibar na Ujumbe ulioongozananao, Mhe: Waziri wa Afya na Utibabu Zanzibar,
Mhe: Naibu Waziri wa Afya na Utibabu Zanzibar Mhe: Mkuu wa Wilaya ya Mjini
Unguja, Muwakilishi wa Shirika la Afya W.H.O, M/kiti wa Baraza la Tiba asili na
Tiba mbadala Zanzibar na wajumbe wa Baraza lako, Itifaki imezingatiwa, Viongozi wa Waganga wa
asili na Waganga wa asili mliohudhuria, wapendwa waalikwa wote Mabibi na
Mabwana Asalamualeikum. (TAIRENI WAGANGA )
Awali ya yote tumshukuru Mola muumba wa Ulimwengu na
vilivyomo ndani yake kwa kutuwezesha kufika hapa tukiwa wazima wa afya, pia
tunamuoba Mola wetu awape afuweni wale wote walishindwa kufika leo hii kutokana
na sababu mbali mbali zikiwemo za maradhi.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi tunapenda kukupa shukrani za pekee kwa
kuwacha shughuli zako za kibinafsi na Kiserikali, kuja kujiunga nasi katika
hafla hii ya madhimisho ya waganga wa asili hongora sana Mama yetu mpendwa.
Pia sijawasahau Wanakamati ya maandalizi na wale wote
waliochangia kwa njia moja au nyengine katika kufanikisha maadhimisho yetu haya
ya leo pia karibuni sana Waganga wenzetu mliotoka Nchi Rafiki za Afrika Mashariki
mnastahili pongezi za dhati kwa ujasiri wenu mlituonesha kufika visiwani kwetu na
huu ndio udugu halisi utakaotufanya tufike tuwendako katika kuziingiza dawa
zetu za asili ndani ya mfumo wa kisasa,
kiuweledi na kiufanisi zaidi.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi chimbuko la maadhimisho haya ni vikao
vilivyotokana na Shirika la Afya Ulimwenguni W.H.O kutowa azimio kuwa Nchi za Kiafrika
ziwezeshwe kuimarisha dawa zao za asili ili kujipunguzia mzigo mkubwa wa
kununuwa madawa ya kisasa ambayo yanahitaji fedha nyingi za kigeni, na ndipo
ilipopangwa siku hii ya waganga wa asili Barani Afrika tokea Mwaka 2003 na hapa
Zanzibar tunaziadhimisha mfululizo tokea Mwaka huo hadi leo, baadhi ya
mafanikio tuliyoyapata ni kama yafuatayo :-
1.
Mashirikiano
makubwa kati ya waganga wenyewe, baina ya Nchi moja na nyengine na hatimae
tumeweza kuunda Umoja wa waganga wa asili wa Afrika Mashariki na kila ifikapo
siku kama hii ya maadhimisho ya waganga ndipo tunapofanya tathmini ya kujuwa
mafanikio, changamoto na matatizo tunayopambananayo.
2.
Pia
tunamashirikiano ya karibu baina ya waganga wa asili na madaktari wa Hospitali
kwa kutupatiya Semina, Mafunzo na kubadilishana ujuzi kati yetu hivyo basi imepelekea
kupeyana rufaa baina yetu, na yale magonjwa yaliyo nje ya uwezo wetu waganga wa
asili kuyapeleka Hospitalini na wao madaktari wa Hospitali yale magonjwa
wanayoyaona yanastahili kwenda kwa waganga wa asili wanatuleteya hivyo kuanza
kuondoka kwa lile Daraja linalotugawa baina ya waganga na madaktari wa Hospitali.
Sasa napenda kuvitaja Vitengo vya Hospitali ambavyo tunashirikianavyo :-
·
Kitengo
cha chakula dawa na vipodozi kinatufanyia
uchunguzi wa dawa zetu kama hazina maradhara na nisalama kwa kula
binaadamu, pia kutuelimisha namna ya utayarishaji bora wa madawa pamoja na kuzifanya
ziuzike Kitaifa na Kimataifa.
·
Kitengo
cha macho kuna ugonjwa unaitwa mtoto wa jicho hospitalini wanaweza sana kwa kumfanyia
mgojwa upasuaji na kuona kama mwanzo hivyo tunakutana kwa semina za kuongeza na
ujuzi wa kimatibabu baina yetu.
·
Kitengo
cha malaria kinatupatia semina za mara kwa mara na kutuelimisha kuwa inapofikia
homa ya mgonjwa kuwa juu inatubidi kumuwahisha hospitalini kwani inaweza
kumpanda kichwani na kuonekana kama mgonjwa wa akili lakini hospitalini anapatiwa
shindano ya kutuliza malaria.
·
Kitengo
cha presha na sukari haya ni magonjwa endelevu ambayo bila ya kuwa na vipimo
vya Kihospitali huwezi kumpatia dawa mgonjwa vile vile inatubidi kutowa rufaa pale tunapoona dawa zetu
hazijampatia nafuu mgonjwa na vipimo bado vinaonyesha ugojwa uko juu sana au
umeshuka sana kiasi ambacho utamleteya
madhara mgonjwa, hospitalini tunajuwa wambinu za hali ya juu na vifaa vya
kimagharibi ambavyo vinakubalika ulimwenguni kote.
Isitoshe kumeandaliwa mradi wa
matibabu ya pamoja baina ya waganga wa asili na kitengo cha presha na sukari
hivyo kwa kuanziya klinik za tiba asili 20 na viringe 5 vimepatiwa vifaa vya
kupima presha na sukari pia kutakiwa kutowa ripoti ya kila miezi 3 - 6 na ya
mwaka kwa lengo la kupunguza athari zinazojitokeza kwa wagonjwa wa sukari na
presha kwani lengo kuu la mradi huu ni kuwapatia mafunzo na vifaa waganga wote
waliosajiliwa na wanaojisshughulisha
kutibu magonjwa ya presha na sukari.
Pia kutokana na magonjwa yenyewe
yalivyo yanapelekea baadhi ya wagonjwa kupata kiharusi hivyo kundi hili la
watibabu wa asili limepatiwa fursa ya kwenda kujifunza kwa vitendo katika idara
ya viungo hospitali ya Mnazimmoja kwa minajili yakutumia mbinu zote mbili za
kiasili na kisayansi
Mhe: Mgeni Rasmi kwaruhusa yako
napenda kuwasimamisha mama Tanjya na mama Karolina ili uwaone hawa ndio
wafadhili wetu wa mradi huu wa presha na sukari hongereni sana kwa mchango wenu
wa hali na mali.
·
Kitengo
cha T/B, Ukoma na Ukimwi haya ni magonjwa thakili sana kwani ni magonjwa
yanayoambukiza hivyo inatulazimu
mashirikiano ya karibu kabisa na madaktari katika kuyatibu kwake.
·
Kitengo
cha Mental mashirikiano yetu ni ya karibu sana pale tunapoona ugojwa wa akili
hautabiriki hivyo mgonjwa anaweza akaanzia upande mmoja wa matibabu na
kumalizia upande wa pili wa matibabu kwani lengo letu ni moja tu kumpatia uzima
mgonjwa pia kumeadaliwa mradi wa ugonjwa wa sonona ambao kwa sasa unaratibiwa
Wilaya ya Kusini Unguja na Kaskazini A Unguja hivyo waganga wa asili wanaoishi
maeneo hayo wamepatiwa semina maalumu za kuutambuwa ugonjwa huo wa sonona na
jinsi ya kuutibu na pale inapoonekana
hali ya mgonjwa inazidi watowe rufaa katika vituo vya Afya vilivyoteuliwa
kutibu magonjwa hayo ndai ya Wilaya zao na fomu za rufaa wamepatiwa.
Na sisi waganga wa asili tunatowa pongezi kwa madaktari wa
Hosptali ya akili na Wafadhili wao kwa kutowa wazo na kuona iko haja ya waganga wa asili kupatiwa Wodi
ya kuwatibu wagonjwa wa akili ndani ya Hospitali ya Mental kwa kweli ni suala
la kupigiwa mfano na kuviomba vitengo vyengine kuiga mfano wao.
·
Kitengo
cha mama na watoto tuna wakunga wa asili ambao wanauzowefu mkubwa wa kuleya
mimba kwa mjamzito mpaka kuzalisha, kutibu watoto lakini bado kunahitajika
vipimo vya kisayansi na mbinu mbadala za madaktari wetu mahiri wa kihospitali
hivyo lazima mashirikiano kati yao yawepo kwa kiwango kikubwa sana na kuwafanya
wakunga wetu wa asili kufaya kazi zao kwa kujiamini zaidi.
·
Kitengo
cha Benki ya damu, hichi ndio moyo wa
matibabu kwani mgonjwa anapopungukiwa na damu au kuzidiwa na damu inatulazimu
kuupata mchango wao kikamilifu na ndio maana na sisi waganga wa asili
tunaishajiisha jamii kujijengea utamaduni wa kuchangia damu na ukichangia
unakuwa mwanachama na kupatiwa kadi abayo ni rahisi kwa mgojwa wako kupatiwa
damu mara moja pindi inapohitajika.
3.
Vile
vile Jamii imekuwa na uwelewa wa kuziamini na kutumia dawa za asili hivyo
kuwezesha kufunguliwa Kliniki za dawa za asili na Kliniki za tiba mbadala
ambazo kwa sasa zinaendeshwa na rafiki zetu wenye asili ya Eshia kama Wachina
na Wakorea kwani Kliniki hizi zinahitaji elimu ya Kisayansi zaidi Kliniki hizi
zinauwezo wa kutumia hata vifaa vya Kimagharibi katika kuendesha matibabu yake.
Mheshimiwa
Mgeni Rasmi kama tujuavyo kila penye mafanikio kama haya tuliyoyataja hapo juu
huwa hapaachi changamoto na matatizo, kati ya matatizo tuliyonayo ni kama
yafuatayo ;-
1.
Tunawaomba
waganga wenzetu ambao hawajajisajili na Baraza la Tiba Asili wafanye hivyo
kwani kutatuwezesha kupata maendeleo ambayo yalikuwa ndio ndoto zetu za siku
nyingi.
2.
Madawa
tunayoyafanya tunaomba yapatiwe maabara ya utafiti ambayo itaweza kutowa
tathmini ya magonjwa yanayotibiwa na dawa hizo na viwango vya matumizi yake na
sio sasa hivi tunapata majibu ya kuwa salama tu kwa mtumizi ya binaadam huo ni uchunguzi tu na sio utafiti.
3.
Upande wa
Madaktari wa Hospitali bado kuna Madaktari ambao wanauwelewa mdogo wa haya
mashirikiano yetu kwa kuona wanashiriana na waganga ambao hawana elimu kama
waliyonayo wao lakini wajuwe kuitwa kwao Madaktari wa kisasa, kulianzia madaktari
wa zamani nao ni waganga wa asili na utaalamu wao huu wa zamani ndio ulioimarishwa
hatua kwa hatua mpaka ukafikia hapa tunapouona hivi sasa na wao kuitwa madaktari
wa kisasa na kadiri miaka inavyosonga mbele hata ujuzi wao wa hivi sasa utakuwa
wa zamani kama wanavyoudharau utaalamu wa waganga wa asili hivi sasa tunaomba tuondokane
na dhana hizo potofu tushirikiane baina ya waganga wa asili na madaktari wa
hospitalini kwa lengo la kutowa matibabu yaliyo bora ndani ya jamii.
Mheshimiwa
Mgeni Rasmi: Waziri
wa Biashara Viwanda na Masoko Zanzibar
tunakujuwa umahiri wako wa kazi ulionao lakini tunaleta ombi letu kwako utufikishie
salamu zetu kwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi kuwa kunahitajika Bajeti maalum ya Mwaka ujao wa Fedha ili tutafutiwe
Chuo cha Utafiti ambacho kitaweza kufanya utafiti wa madawa yetu bila kwenda
Nchi jirani.
Mheshimiwa
Mgeni Rasmi: sasa kwa ruhusa yako napenda kuitaja kauli mbiu ya Mwaka huu 2018
kama ifuatavyo :-
UTENGENEZAJI WA KIENYEJI WA BIDHAA ZA
TIBA ASILI KATKA KANDA YA AFRIKA,
Kama
inavyosomeka kauli mbiu yenyewe kuwa ni UTENGENEZAJI wa madawa ya asili yaliyo
bora kwani ni ukweli usiopingika kuwa Bara letu la Afrika limebarikiwa miti ya
dawa ya kutosha ukilinganisha na Mabara mengine hivyo kama tutajipanga vizuri
basi tutatengeneza Masoko makubwa ya bidhaa zitokanazo na mimeya ya asili na
kujipatia kipato cha mtu moja moja na Taifa kwa ujumla lakini haya yote
yatafanikiwa kama tutaunganisha ujuzi wetu, vitendea kazi na mitaji ya kuongeza
thamani madawa yetu ya asili.
Tunamuomba
Mola wetu aturejeshe majumbani kwetu salama usalimini.
Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Zanzibar
Asanteni kwa kunisikiliza
Mtayarishaji
HAJI
JUMA MSANIF
KATIBU
MKUU JUTIJAZA
MWISHO
No comments:
Post a Comment