Habari za Punde

Mchezo wa Fainali ya Kombe la FA Kati ya KMKM na Jamuhuri Kufanyika Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba Kesho.

Fainali ya Kombe la FA Zanzibar itachezwa kesho kati ya Jamhuri dhidi ya KMKM saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.

Bingwa wa Kombe hilo atapata nafasi ya kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya JKU utakaochezwa Oktoba 18, 2018 saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Amaan.

Tumezungumza na afisa habari wa ZFA Abubakar Khatib Kisandu na hapa akituelezea maandalizi ya mwisho kuelekea fainali hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.