1Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mhe. Japhet Hasunga (katikati) akiwa na Mkuu wa mkoa wa
Lindi, Godfrey Zambi wakiwa wameongozana na Wakurugenzi pamoja na Wazee wa kabila la
Wamwela wakati kutembelea nyumba ya kabila la Mwela katika kijiji cha
Makumbusho kabla ya kufunga tamasha la utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na
jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku nne katika kijiji hicho
jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na Athumani Issa wakati alipotembelea
nyumba ya kabila la Wamwela katika kijiji cha Makumbusho wakati wa kufunga tamasha la
utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika
kwa muda wa siku nne katika kijiji hicho
jijini Dar es salaam
Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mhe. Japhet Hasunga akiwasaidia akina Mama wa kabila la
Wamwela kutwanga nafaka wakati alipotembelea nyumba ya kabila la
Wamwela katika kijiji cha Makumbusho wakati wa
kufunga tamasha la utamaduni wa
mtanzania inayowakilishwa na jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa
siku nne katika kijiji hicho jijini Dar es salaam
Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mhe. Japhet Hasunga akipewa kibuyu chenye pombe na Halima Abdallah ambacho kimekuwa
kikitumiwa na kabila hilo kunywea pombe
wakati alipotembelea nyumba ya kabila la Wamwela katika kijiji cha
Makumbusho wakati wa kufunga tamasha la utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na
jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku nne katika kijiji hicho
jijini Dar es salaam
Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mhe. Japhet Hasunga akiangalia baadhi ya mabaki ya samaki
aina ya nguva aliyekutwa amekufa kando kando mwa bahari ya Hindi mkoani Lindi
wakati alipotembelea mabanda kabla ya kufunga tamasha la utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na
jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku nne katika kijiji hicho
jijini Dar es salaam.
- Baadhi ya vikundi vya ngoma vikitumbuiza wakati
wa kufunga tamasha la utamaduni wa mtanzania
inayowakilishwa na jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku
nne katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam
( Picha na Lusungu Helela)
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Japhet Hasunga amewashauri wasanii wanaopiga picha za utupu waache kupiga picha hizo badala yake watembelee Hifadhi za Taifa ili wakapige picha na simba, twiga chui pamoja na sokwe kwa ili waweze kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini.
Pia amewataka wasanii wenye nia ya kutaka kutengeneza filamu katika Hifadhi ya Taifa wawasaliane na Uongozi wa Hifadhi za Taifa au wawasiliane na yeye mwenyewe moja kwa moja.
Ametoa rai hiyo wakati akifunga tamasha la utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku nne katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam
Aidha, Ameiasa jamii iitumie mitandao ya kijamii kujipatia elimu badala ya kusambaza picha ambazo ni kinyume cha maadili ya Mtanzania.
Ameongeza kuwa Jamii iwakemee wasanii wenye tabia hiyo badala ya kusubilia Serikali ndo ichukue hatua.
No comments:
Post a Comment