Baadhi ya
mabaki ya Mjusi mkubwa mwenye urefu wa mita 13.7 kwenda juu
aliyegunduliwa miaka 100 iliyopita katika eneo la Tendaguru mkoani Lindi
aliyepo katika makumbusho nchini Ujerumani ambao kwa sasa Serikali ya Tanzania
imeanza mazungumzo kuona jinsi gani itaanza kupata gawio lake kupitia watalii.
Mjusi
huyo kwa jina la kitaalamu anaitwa Dinosaur ambapo mabaki yake yalivumbuliwa miaka
100 iliyopita katika eneo la Tendaguru
mkoani Lindi, yalikusanywa na kupelekwa nchini Ujerumani ambako wataalamu waliyaunda
na kisha kuyaweka kwenye Makumbusho hiyo.
Amesema
lengo la mazungumzo hayo ni kutaka kujua
kiasi gani cha mapato yanayokusanywa
na namna gani wanavyoweza kugawana mapato hayo yatokanayo na watalii kupitia mjusi huyo
baina ya Serikali hizo mbili.
Amesema
mwelekeo wa mazungumzo hayo yaitapelekea
Serikali ya Tanzania kufanya uamuzi wa
kumrudisha mjusi huyo au kumuacha kule
kule lakini akiwa analiingizia pato taifa
Ameyabainisha
hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana
na mIkakati ya Serikali ya kuendeleza
vivutio vya utalii kwa mikoa ya Kusini.
Hata hivyo, Mhe.Hasunga amesema uamuzi wa kumrudisha mjusi huyo nchini utakuwa mgumu kwa vile
sehemu kubwa ya mjusi huyo ameunganishwa unganishwa kwa kutumia vifaa maalumu.
Ameongeza
kuwa kutokana na jinsi alivyounganishwa unganishwa na anakadiri wa kuwa na urefu wa mita 13.7 kwenda juu hivyo kumsafirisha itakuwa ngumu.
Katika
hatau nyingine, Mhe Hasunga amesema hadi hivi sasa Serikali ya Ujerumani haijaweza kuweka bayana
kiasi cha mapato yanayokusanywa kupitia
Mjusi huyo licha ya kuwa Serikali hiyo
imekuwa ikifadhili miradi mingi ya uhifadhi nchini.
"Tunaamini
kuwa pesa wanazofadhili miradi mingi ya Uhifadhi imekuwa inatokana na makusany okupitia
Mjusi huyo Mkubwa" amesema Hasunga
Hata
hivyo,kuendelea kuwepo kwa masalia ya mjusi huyo katika Makumbusho hiyo kuna
manufaa makubwa kwa vile anatambuliwa kuwa ni wa kutoka Tanzania,Hivyo ni
Balozi wa Utalii na utafiti wa kisayansi anayeitangaza Tanzania sehemu
mbalimbali duniani.
No comments:
Post a Comment