Muonekano wa barabara ya Morogoro eneo la Kimara mwisho Jijini Dar es salaam hivi leo ambapo tayari maandalizi ya ule mradi wa ujenzi wa barabara ya njia sita kutoka Ubungo hadi Kibaha Mkoani Pwani yenye urefu wa kilometa 16 umeiva. Ujenzi wa barabara hiyo unaotarajia kuanza mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu utasaidia kukuza uchumi kwa kuongeza kasi ya usafirishaji wa bidhaa katika nchi jirani kupitia bandari ya Dar es Salaam. Pia inatarajiwa utasaidia kupambana na changamoto ya msongamano wa magari na kuziwezesha barabara zote za Jiji la Dar es Salaam kupitika katika majira yote ya mwaka. Picha na IKULU
Miaka kumi ya mabadiliko ya kimfumo katika usimamizi na uthibiti wa taka
nchini Tanzania
-
Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri Duniani, tunajivunia kuadhimisha
miaka 10 ya mabadiliko ya kimfumo katika usimamizi na uthibiti wa taka
nchini T...
31 minutes ago
No comments:
Post a Comment