Habari za Punde

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Afanya Ziara Kisiwani Pemba.

NAIBU Waziri wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhandisi Atashasta Nditiye akiwasili katika uwanja wa ndenge wa Pemba Airport, kwa ziara ya kuangalia maeneo ambayo miwasiliano ya simu hayapatikani katika Mkoa wa Kaskazini Pemba
AFISA Mdhamini Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba Hamad Ahmed Baucha, akiutambulisha ugenzi wa Wizara ya Uchukuzi Mawasiliano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati ulipofika kwa mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla, Katikatiugenzi huo ukiongozwa na Naibu waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Atashasta Nditiye
MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe.Hemed Suleiman Abdalla wanne kutoka kushoto, akiwa na Naibu waziri wa Wizara ya Uchukuzi Mawasiliano ya Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Atashasta Nditiye wakati wa picha ya pamoja baada ya ujumbe wa naibu huyo kujitambulisha katika ofisi hiyo ya mkuu wa Mkoa
NAIBU waziri wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Atashasta Nditiye, akizungumza mara baada ya kukikagua kituo cha Tehama kilichopo katika Ofisi ya Tawala za Mikoa Machomanne Chake Chake Pemba
MBUNGE wa Viti maalumu Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe. Maida Hamad Abdalla, akutambulisha ugeni wa Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiongozwa na Naibu waziri wa Wizara hiyo Mhe.Atashasta Nditiye uliofika katika Shehia ya Kiungoni juu ya Kuangania upatikanaji wa mawasiliano ya simu
NAIBU waziri wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Atashasta Nditiye, akizungumza na wananchi wa shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete, juu ya ukosefu wa mawasiliano ya siku katika shehia hiyo, wakati alipofanya ziara ya kuangalia maeneo ambayo usikivu wake wa mawasiliano mdogo sana
MKURUGENZI wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhandisi Piter Ulanga akizungumza na wananchi wa Shehia ya Kiungoni, baada ya kusikia kilio cha ukosefu wa usikivu wa mawasiliano ya simu katika shehia hiyo
SHEHA wa shehia ya Kiungoni Omar Khamis Othman, akizungumza na waandishi wa habari kutoka Vyombo mbali mbali vya habari, juu ya uwepo wa usikivu mdogo wa mawasiliano ya simu katika shehia yake
MKUU wa WIlaya ya Micheweni  Bi.Salama Mbarouk Khatib, akizungumza juu ya hali ua usikuvu hafifu ya mawasiliano ya simu kwa wananchi wa Wilaya ya Micheweni, wakati wa kikao na Naibu waziri wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Atashasta Nditiye, huko katika skuli ya sekondani Wingwi.
Picha na Abdi Suleiman -Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.