MKURUGENZI
Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), Juma Ameir Hafidh akikanusha
taarifa zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kutolewa kwa
namba mpya za wateja wa benki hiyo. taarifa hiyo aliitoa katika Ofisi za PBZ ziliopo Mpirani Mjini Unguja.
Kulikuwa na Taarifa zilizokuwa zikienea kwenye mitandao ya kijamii kwamba kuanzia jana Jumatatui 03/12/18 PBZ iliingia katika mfumo mpya wa kisasa wa kutunza taarifa za kibenki na hivyo namba za zamani za akaunti hazitumiki tena.
Hata hivyo taarifa hizo si za kweli kama ilivyothibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji PBZ.
NA MWASHAMBA JUMA
BENKI ya Watu wa Zanzibar PBZ
imekanusha taarifa zilizoenea kwenye mitandao jamii kuhusiana na marekebisho
yaliyofanywa hivi karibu na benki hiyo.
Akitoa
taarifa kwa vyombo vya habari hapo ofisini kwao Mpirani, Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki hiyo, Juma Ameir Hafidh aliwataka wananchi na wateja wa benki hiyo
kuupuuza uvumi huo na kusema kuwa hauna ukweli wowote.
Alisema
PBZ ni benki ya Serikali hivyo taarifa zake haziwezi kutolewa mitaani bila
kufuata utaratibu rasmi wa utoaji taarifa sahihi.
“Hii
ni benki ya serikali taarifa zetu haziwezi kuwa za mitaani, hivyo tunawaomba
wananchi wazipuuzie taarifa zisizo rasmi ambazo zimezagaa kwenye mitandao” alitahazarisha
Mkurugenzi huyo.
Aidha,
alieleza hivi karibuni Benki hiyo ilifanya mabadiliko ya mtandao mpya wa
kutolea huduma za kibenki kwa lengo la kuboresha huduma bora kwa wateja wake.
Alisema
mabadiliko yaliyofanywa na benki hiyo hayatoathiri miamala yoyote ile ikiwemo
kutoa na kuweka fedha kwa kutumia akauti za zamani za wateja wake.
“Wateja wote wa benki yetu wataendelea kupata
huduma kama kawaida kwa kutumia akauti zao za zamani, aidha, huduma za hundi na
kadi za ATM zitaendelea kutumika zile zile” alifahamisha Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi
huyo, aliwatoa wasiwasi wateja wa benki hiyo na kueleza kuwa PBZ itaendelea
kuwa benki ya watu wa Zanzibar kwa kutoa huduma bora kwa wateja na wasiokuwa
wateja wake.
Kufuatia
PBZ kuingia katika mfumo mpya wa kisasa, tokea ulipoanza rasmi Disemba tatu
mwaka huu, alisema sasa benki hiyo inatoa huduma ya ‘PBZ Instant Pay’ ambayo
inamuwezesha mteja wa benki hiyo kutumia fedha ndani ya Tanzania ya malipo ya papo
kwa papo.
Aliongeza
kuwa huduma hiyo pia itamuwezesha mtumiaji wa PBZ kutuma pesa hata kwa mtu asiekua
mtejawa PBZ sambamba na kuchukua fedha katika tawi lolote la benki hiyo.
Akizungumzia
mfumo wa ATM alisema wateja sasa wanaweza kutoa fedha kwa masaa 24 bila ya
kuwepo kwa usumbufu wowote pamoja na kutuma, kuhaulisha pesa kutoka akaunti zao
na kwenda katika akaunti ya mteja mwengine wa PBZ.
Huku
mtumiaji wa simu za mkononi mwenye tigopesa, M pesa ama Aitel Money pia atakuwa
na uwezo wa kutoka fedha katika ATM za PBZ.
Akizungumzia
huduma za “Internet Banking” pia alieleza kuwa ni moja ya maboresho mapya
yaliyofanywa na benki hiyo, ambapo alieleza kuwa wateja wao watakuwa na uwezo
wa kutuma fedha katika akaunti za ndani za PBZ na benki nyengine zilizopo
Tanzania, pamoja na kumuwezesha mteja wa benki hiyo kufanya malipo kwa wazabuni
wenye akaunti katika benki hiyo na benki nyengine za ndani na nje
ya nchi.
Aidha,
huduma nyengine ni kumuwezesha mwajiri kulipia mishahara ya wafanyakazi wake
ambao wana akaunti katika benki yoyote iliyopo Tanzania pamoja na wateja kupata
huduba za PBZ pasipo kufika matawini.
No comments:
Post a Comment