Habari za Punde

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA WAZIRI MKUU WA MISRI DKT. MOSTAFA MADBOULY WASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA UJENZI WA MRADI WA KUZALISHA UMEME MEGAWATI 2100 KATIKA MTO RUFIJI, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji kati ya Waakilishi wa Kampuni ya J.V Arab Contractors/El Sewedy Electric pamoja na Waakilishi wa Shirika la Umeme nchini Tanesco.


Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya Utiaji saini wa  Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha Umeme katika mto Rufuji, Mkataba ambao umesainiwa leo 12 Disemba ,2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam, kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya ujenzi  ya Arab Constructor kutoka  nchini Misri.
Waziri Mkuu wa Misri Mustapha Madbouly akiongea  katika Hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa mradi wa umeme katika mto Rufuji uliosainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya Ujenzi kutoka nchini Misri(Arab Constructors)  Ujenzi utakaochukua takribani miaka mitatu kukamilika kwake na kuweza kutoa megawati za umeme 2115.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu wa Misri Mustapha Madbouly (wa tatu kushoto), Makamu wa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan( wa tatu kulia), Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa(wa pili kushoto) na Spika wa Bunge la Mungano wa Tanzania Job Ndugai (wa pili kulia), wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mawaziri na Manaibu Waziri baada ya Hafla fupi ya utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa mRdi wa umeme wa mto Rufiji, mkataba uliosainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya ujenzi kutoka Misri Arab Constructors leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt.John Pombe Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na  Wajumbe wa Kamati ya majadiliano ya Mkataba wa   Ujenzi wa Mradi wa bwawa la umeme mto Rufiji  mara baada ya hafla ya utiaji saini ya ujenzi wa mradi huo uliofanyika Ikulu  Jijini Dar es  Salaam leo 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt.John Pombe Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Wakuu wa Mikoa mbalimbali mara baada ya hafla ya utiaji saini ya ujenzi wa mradi wa umeme wa mto Rufuji uliosainiwa kati ya  Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Ujenzi ya  Arab Contructors kutoka nchini Misri leo 12 Disemba , 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.