Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein Awasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar Akitokea Nchini Uingereza leo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, alipowasili Uwanja wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, akitokea Nchini Uingereza.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe. Said Hassan Said, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Uingereza leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama Zanzibar, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Uningereza leo.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amerudi nchini leo akitokea Uingereza.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume viongozi mbali mbali wa Serikali, vyama vya siasa pamoja na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd walimpokea Rais Dk. Shein.

Wakati huo huo, Rais Dk. Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mazoezi ya viungo kwa wananchi wote yatakayofanyika kisiwani Pemba ambayo yataanzia Wawi Matrekta hadi uwanja wa Gombani.

Mazoezi hayo yatafanyika siku ya Jumaane Januari 1, 2019 ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964.

Siku hiyo hiyo, mnamo majira ya saa kumi za jioni Rais Dk. Shein atafungua skuli ya Msingi Chimba iliyopo Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Jumaatano ya tarehe 2 Januari 2019 saa nne za asubuhi Rais Dk. Shein anatarajia kuzindua vituo vya Uokozi vya KMKM kwa niaba ya Vituo vya Uokozi vya KMKM vya Kiweni na Nungwi hafla itakayofayika  katika Bandari ya Mkoani Pemba.

Uwanja wa Michezo wa Mao-Tse Tung uliopo Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja utafunguliwa na Rais Dk. Shein siku ya Alhamis ya Januari 3, 2019 mnamo majira ya saa kumi za jioni.

Aidha, Rais Dk. Shein ataifungua Barabara ya Kijitoupele hadi Fuoni Mambosasa iliyopo Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini Magharibi mnamo siku ya Jumaamosi ya tarehe 5 Januari 2019 mnamo saa nne za asubuhi.

Rais Dk. Shein ataweka Jiwe la Msingi katika jengo la Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati pamoja na ZURA lililopo Maisara, Wilaya ya Mjini Unguja mnamo siku ya Jumaapili ya Januari 6, 2019.

Jumanne ya Januari 8, 2019 Rais Dk. Shein anatarajia kufungua Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyopo Maruhubi, Wilaya ya Mjini Unguja.

Pamoja na hayo, Rais Dk. Shein anatarajiwa kufungua Skuli ya Sekondari ya Bwefum Wilaya ya Magharibi B Unguja mnamo siku ya Jumaatano ya Januari 9, 2019 ambapo jioni yake anatarajia kutoa nishani hafla itakayofanyika  katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.

Kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar zitafanyika siku ya Jumaamosi ya Januari 12, 2019 katika uwanja wa Gombani uliopo Chake Chake Pemba ambapo Rais Dk. Shein atakuwa mgeni rasmi.

Mnamo majira ya saa mbili za usiku siku hiyo hiyo ya Januari 12, 2019 Rais Dk. Shein atakuwa Mgeni Rasmi katika Taarab Rasmi ya Kikundi cha Taifa itakayofanyika katika kiwanja cha Kufurahishia Watoto cha Tibirinzi kiliopo Chake Chake Pemba.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.