Dkt. Flora Kessi, Mkuu wa Chuo cha Afya Ifakara, alikwasilisha mada wakati wa kikao hicho cha siku moja kwenye ukumbi wa Edema mjini Morogoro
Baadhi ya wajumbe wa Bodi (Consortium),wakimsikiliza Bi Jackie Patrick aliyesimama wakati wa kikao hicho cha siku moja cha kujengeana uwezo.
Baadhi ya Washiriki wa Semina hiyo ya Maboresho ya Mitaala ya Afya kuhusu suala la Takwimu wakisiliza kwa makini mtoa Mada hayupo pichani.
Dkt. Michael Msende, kutoka chauo cha Serikali za Mitaa Hombolo akichangia mada wakati wa Semina hiyo yakupitia mapendekezo ya mchakato wa maboresho ya mitaala ya kada za Afya. (Picha zote na Atley Kuni-TAMISEMI)
Na. Atley Kuni-
Morogoro.
Jopo
la Wataalam kutoka Idara Mbali Mbali za Serikali wakiongozwa na Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Wizara ya Afya, wanakusudia
kuboresha Mitaala ya Vyuo vya elimu ya Afya huku nguvu kubwa ikielekezwa katika
matumizi sahihi ya takwimu zipatikanazo kutoka katika vituo vya kutolea huduma za
afya na matumizi yake.
Wadau
hao waliokutana kwa siku moja mjini Morogoro, walisema kwa muda mrefu takwimu
nyingi zinazopatikana kutoka katika vituo vya kutolea huduma zimekuwa
zikukusanywa kwa mazoea na hivyo kubaki bila kutumika katika ngazi mbali mbali
za maamuzi.
Akizungumza
kwa niaba ya Mkurugenzi wa TEHAMA OR-TAMISEMI, Afisa TEHAMA, Melkiory Baltazari
alisema, taaluma bora ni ile inayotafsiri maendeleo ya watu kwa vitendo na
maendeleo hayo kuisaidia jamii.
“Tunazalisha
data nyingi sana, lakini kiwango cha matumizi ya data hizo hakikidhi viwango
tunavyo hitaji hususa ni katika ngazi za maamuzi alisema Baltazary na kuongeza
kuwa, ukimfunza mtu, halafu taaluma yake hiyo ikatumika vizuri kwa kile kilicho
kusudiwa utaona thamani ya elimu husika”.
Naye
Mtaalam kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Issa Mbaga, alisema, umefika wakati suala
la data likaingizwa katika mitaala ya vyuo vya wataalam wa Afya ili kuwajengea
utamaduni wakuthamini takwimu pindi wawapo katika utekelezaji wa majuku yao ya
kila siku.
Akizungumza
wakati wa kutoa salaam za mradi wa PATH Tanzania, Mkurugenzi wa mradi wa Data Use Partnership Bi. Jackie Patrick,
alisema anaipongeza Serikali kwa kuamua kuboresha suala la mifumo na matumizi
ya takwimu kwa mapana yake kama yalivyoainishwa kwenya “Tanzania Digital Health Investments Roadmap 2017-2013”
“Sisi
tunaipongeza sana Serikali ya awamu ya tano kwa namna inavyo weka msisitizo
katika matumizi ya takwimu hususani zile tunazo zipata kutoka katika vituo vya
kutolea huduma. Pia naipongeza serikali kwa kuamua kutumia ubunifu wa hali ya juu
kujengea uwezo wa wahudumu wa afya kwa kuanzisha “Data Use Capacity Building Consortium” kupitia mradi wake wa Data Use Partnership ulioko chini ya
wizara ya afya na Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Alisema Bi. Jackie na kuongeza
kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi chache Afrika kama sio pekee inayotumia
ubunifu huu wa hali ya juu wa kutumia muungano “consortium” wa taasisi za kitafiti na taasisi za mafunzo za ndani
ya nchi kujenga uwezo wa wahudumu wa afya kwenye matumizi ya takwimu. Huu ni
ubunifu wa gharama nafuu na wa kudumu katika sekta ya afya” alihitimisha
Kando
ya mafunzo hayo yakuwajengeana uwezo wataalam hao, Mkuu wa Chuo Uuguzi Ifakara,
Prof. Florah Kessi, aliwaambia waandishi wa habari kwamba, lengo la Mafunzo
hayo ni kuondokana na kufanya kazi kwa mazoea.
“Katika
Mpango wa sasa, tunataka watoa huduma wanao ingia vyuoni na wale waliomaliza vyuo
lazima sehemu ya mitaala yao, soma la ‘data
use’ lipewe kipaumbele, maana walio wengi wanakusanya data lakini hawazitumi.
” alisema Prof. Kessy na kuongeza kuwa, mara
kwa mara nimekuwa nikimsikiliza Mhe. Rais kwenye hutuba zake, kubwa
analolifanya nikuongea kwa kutumia takwimu, lakini halikadhalika Mawaziri,
Wabunge na viongozi wengine pia hawajaacha kutumia takwimu katika hotuba zao”.
Kwa
upande wao washiriki wa semina hiyo, walisema wakati wa maboresho ya mitaala
hiyo upo umuhimu wa kuwahusisha wataalam wa afya waliopo kazini ambao wana
uzoefu lakini pia kutambua matumizi ya data walizo nazo.
“Tunapo
andaa mitaala hii kwaajili kuiboresha mitaala yetu, tusiache kuwahusisha
wakusanyaji, lakini pia watumiaji wa siku kwa siku ili kujiridhisha kwenye
uhalisia wa data.” Alinikuliwa Faraja Makafu kutoka NACTE.
Akifunga
Semina hiyo ya siku moja ya kujadili matokeo yaliyopatikana baada ya mchakato
huo wakujadili kozi za muda mfupi na zile za muda mrefu kwa watumishi waliopo makazini
na wale wanaojiunga na vyuo Mkurugenzi msaidizi wa huduma za afya Dkt. Anna
Nswira kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, alisema katika hali ya sasa, mtaalam wa
afya ndio Mchumi, Mwalimu, Mhandisi na ndio mwanasheria na taaluma zingine,
hivyo wakati nchi inahubiri suala la uchumi wa viwanda hatutafikia huko kama
wananchi watakuwa hawana afya njema.
Kukamilika
kwa mtaala huo na kuanza kutumika katika vyuo vya kati na vyuo vikuu itasaidia
kuimarisha matumizi ya data katika ngazi mbali mbali za maamuzi hususan wakati
wa kupanga.
Jumla
ya Washiriki 153 kutoka taasisi mbali mbali za Serikali wamehudhuria katika
semina hiyo.
No comments:
Post a Comment