Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wanachama wa CCM Mkoa wa Magharibi Unguja katika ukumbi wa Afisi ya CCM Mkoa wa Mjini Amani wakati wa ziara yake katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja kutembelea Miradi ya Maendeleo
Na.Abdi Shamnah.Ikulu Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein , akiwa
pia ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, alizungumza na Viongozi wa Wilaya ya
Dimani Kichama, Kamati za Siasa za Mkoa Magharibi, Kamati za siasa za Wilaya
pamoja an viongozi mbali mbali wa chama hicho, katika ukumbi wa CCM Mkoa,
Amani.
Akizungumna
wanachama hao, Dk. Shein alisisitiza haja ya kuwepo umoja na mshikamano ndani
ya chama hicho ili kujenga chama bora kitakachohakikishia ushindi katika uchaguzi
mkuu ujao wa 2020.
Alisema
nguvu za chama hicho ni umoja, hivyo akawataka wanachama kuendelea
kushikamana na kuepuka mifarakano na
utengano, huku akiwataka wanachama kufuata maadili ya chama hicho katika
kushajiisha umoja.
Alisema
huu ni wakati ambao umoja unahitajika
zaidi ili kuwa katika mazingira bora kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020.
Alisema
katiba ya CCM imeweka wazi dhamira ya chams hicho kushinda katika chaguzi zote
, ili kuendleea kushika dola na kuongoza Serikali.
Alisema
ili kufikia hatua ya ushindi ni lazima CCM iendelee kushika mpini, akiweka
bayana kuwa mpini huo utashikwa na watu wenye umoja, wanaozingatia maadili na
wasio na tamaa.
Alisema
Serikali ya Mapinduzi inayoongozwa na CCM ilianza maadalizi ya uchaguzi huo
mara tu baada ya uchaguzi wa marudio wa 2016 kwa kuandaa mpango wa utekelezaji
wa Ilani,
Alisema
serikali imejitahidi kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji wa Ilani kwa
kufanikisha miradi mbali mbali ya maendeleo, ikiwemo sekta za maji, barabara,
afya na elimu.
Alisema
baadhi ya viongozi ikiwemo Wabunge na Wawakilishi hawana habari kabisa na
utekelezaji wa Ilani, hivyo akawataka kuwa imara na kutekeleza kwa vitendo
ilani ya chama hicho.
Aidha,
aliwataka kutumia vyema muda uliobaki kwa kutekelza ahadi walizozitowa kwa wapiga
kura wao ,
Mapema,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,
Abdalla Juma Sadala alisema Uongozi wa Chama Wilaya Dimani umefanya
juhudi kubwa za kuwafikia wnaachama wake hadi ngazi za chini pamoja na kutatuwa
changamoto mbali mbali ziilizojiri.
Aliwataka
viongozi hao kuhakikisha wanatekeleza ahadi walizozitoa kwa wapiga kura wao,
Aidha,
taarifa ya Chama Wilaya hiyo, imebainisha wanachama 27,272 wameandikishwa
Wilayani humo, huku asilimia sita ya wanaachama hao wakiwa tayri wamelipa ada
za uanachama zilizofikia zaidi ya shilingi Milioni 2.5
No comments:
Post a Comment