Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Basraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, Akiwa Katika Ziara Yake Wilaya ya Magharibi B Unguja Aweka Jiwe la Msingi Majengo ya Skuli ya Msingi ya Kwarara leo.

Moja ya Majengo Matatu ya Kisasa ya Skuli ya Msingi ya Kwarara yanayojengwa kwa kushirikiana na Wahisani Wakubwa Shirika la "Good-Neighbors" kutoka Nchini ya Jamuhuri ya Korea ya Kusini inayojengwa katika maeneo ya Kwarara Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Kichama Ndg. Mohammed Rajab Soud, alipowasili katika viwanja vya Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Msingi ya Kisasa huko Kwarara Zanzibar, akiwa katika ziara yake katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la "Good -Neighbors" kutoka Jamuhuri ya Watu wa Korea ya Kusini, alipowasili katika viwanja vya Mradi wa Skuli ya Kisasa ya Msingi ya Kwarara Wilaya ya Magharibi B,Unguja leo, 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiondoa kipazia kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Ujengi wa Skuli ya Msingi ya Kwarara Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Mama Mwanamwema Shein, kushoto na kulia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma, wakipiga makofi baada ya hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Skuli ya Msingi ya Kwarara Wilaya ya Magharibi B, Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, Mama Mwanamwema Shein, wakimsikiliza Msanifu Majengo wa Kampuni ya SRAT Consult Ndg Salim Rajab.Twakyondo, akitowa maelezo ya michora ya ujenzi huo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, Mama Mwanamwema Shein, wakimsikiliza Msanifu Majengo wa Kampuni ya SRAT Consult Ndg Salim Rajab.Twakyondo, akitowa maelezo ya michora ya ujenzi huo.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bi. Madina Mjaka, alitowa taarifa ya Kitaalam ya Ujenzi wa Majengo ya Skuli hiyo ya Msingi ya Kwarara Zanzibar, wakati wa hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika ziara yake katika Wilaya ya Magharibi B, Unguja. 
Waziri wa Elimi na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma, akizungumza wakati wa hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Msingi ya Kwarara inayojengwa na Shirika la " Good-Neighbors" kutoka Jamuhuri ya Watu wa Korea ya Kusini, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Kwarara leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Aliu Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Kisasa ya Msingi Kwarara Zanzibar, akiwa katika ziara yake katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiwa katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la Mradi wa Skuli ya Kisasa ya Msingi Kwarara Wilaya ya Magharibi B, Unguja kulia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma na kushoto Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dr, Abdallah Juma Mabodi na Meya wa Manispa ya Magharibi B. Ndg.Mabadi, wakifuatilia hafla hiyo.







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.