Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii
Tanzania Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akitia saini kwenye karatasi ya makubaliano
ya ushirikiano wa maandalizi ya maonesho ya ngumi ya kimataifa yatakayoambatana
na Mkutano wa Wafanyabiashara na Watalii kutoka katika mataifa 75 Duniani
utakaofanyika mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu 2019,kushoto kwake ni Makamu
wa Rais wa Kampuni ya Rejoy ya China inayoandaa mashindano hayo Bw. Andrew Lu
Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania Jaji
Mstaafu Thomas Mihayo na Makamu wa Rais wa Kampuni ya kimataifa ya Rejoy ya
nchini china wakionyesha karatasi za makubaliano ya ushirikiano wa maandalizi
ya mchezo wa ngumi wa kimataifa utakaofanyika Jijini Arusha mapema mwezi Julai
mwaka huu
Na Grace Semfuko-Maelezo
Bodi ya Utalii Tanzania TTB imetiliana saini
mkataba wa ushirikiano na Taasisi ya Rejoy ya Beijing Nchini China ya
maandalizi ya mikutano mikubwa ya siku mbili ya wafanyabiashara wa sekta
mbalimbali wa nchi hizo wakati wa msimu wa maonesho ya kimataifa ya mchezo wa
ngumi yanayotarajiwa kufanyika Jijini Arusha mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka
huu.
Mkataba huo unahusisha maandalizi
ya mikutano ya washiriki wa maonesho hayo, ambapo wafanyabiashara na Watalii
kutoka katika Nchi zaidi ya nchi 75 Duniani wanatarajiwa kushiriki maonesho
hayo yatakayoambatana na kutembelea vivutio vya utalii pamoja na kubadilishana
uzoefu wa kibiashara baina ya watu wa mataifa hayo.
Akizungumza mara baada ya
kutiliana saini makubaliano hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya TTB Jaji Mstaafu Thomas
Mihayo, alisema ni hatua muhimu kwa Tanzania ya kupokea ugeni huo ambao pamoja
na kunufaisha Taifa kiuchumi lakini pia utatangaza Tanzania katika utalii.
“Sisi Bodi ya Utalii Tanzania ni
furaha yetu kuona tumefikia makubaliano haya ambayo yataleta tija kwa Taifa
letu, Kampuni ya Rejoy ni ya kimataifa ambayo imepewa idhini ya kuandaa mchezo
wa ngumi Duniani, ni kampuni kubwa, maarufu na yenye uzoefu wa kutosha katika
mchezo huo, hivyo kuja kwao Tanzania ni hatua kubwa sana,pia Ukumbi wa mikutano
Arusha AICC wanahusika katika makubaliano haya” alisema Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB
Makamu wa Rais wa Kampuni ya
Kimataifa ya Rejoy, Bw. Andrew Lu, ambayo wemekuwepo nchinikwaa wiki sasa, alisema makubaliano hayo yanalenga
kuwaweka karibu TTB na Kampuni yake na kwamba watahakikisha maandalizi ya
mikutano na mchezo huo wa ngumi yatafanikiwa kwani wameweka hamasa kubwa kwenye
nchi zilizoonyesha nia ya kushiriki.
“Tunautangaza mchezo huo kwa hapa
Tanzania, watu wengi watakuja kushiriki na kuuona, pia tunatangaza utalii wa
Tanzania ili watu hao wakija waweze pia kutembelea hifadhi za utalii na vivutio
vya Taifa la Tanzania, tuna uzoefu wa miaka 15 katika kazi hii na tutafanikiwa”
alisema Andrew Lu Makamu wa Rais wa Kampuni ya kimataifa ya mchezo wa ngumi.
Makubaliano hayo ambayo mchakato
wake unaanza February 22 na kutarajiwa kukamilika machi mwishoni, utekelezaji
wake utaanza mwezi April kwa maandalizi ya kupokea ugeni huo mkubwa huku mwezi
julai mwanzoni Tanzania ikitarajiwa kupokea ugeni huo kutoka katika mataifa
mbalimbali, zaidi ya 70 duniani.
Katika tukio kubwa hilo la ngumi
za uzito wote ambalo litarushwa mubashara nchi nying duniani litatizamwa na
maelfu ya wahudhuriaji toka china na nchi mbalimbali wakiwaa ni watalii na
wafanya baishara kama wasafirishaji na wahudumiaji katika sekta ya utalii lengo
likiwa ni kutangaza sekta ya utalii duniani.
No comments:
Post a Comment