Mratibu
wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (
MKURABITA) Bi Seraphia Mgembe akionesha
hati milki ya kimila ya kumiliki ardhi na kusisitiza umuhimu wa wananchi
Wilayani Chamwino mkoani Dodoma kuchukua hati milki hizo baada ya kurasimisha mashamba yao ili waweze
kujiletea maendeleo.
Meneja
Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara
za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) Bw. Antony Temu akisisitiza umuhimu wa mafunzo
ya kuwajengea uwezo wananchi waliorasimisha mashamba yao katika kijiji cha
Membe Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Afisa
Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Chamwino
Bi Juliana Mtolera akisisitiza jambo wakati wa mafunzo kwa wakulima zaidi ya
100 katika kijiji cha Membe Wilayani humo wakati wa mafunzo yakuwajengea uwezo
ili waweze kuzalisha kwa tija, mafunzo hayo yameandaliwa na Mpango wa
Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania ( MKURABITA) kwa
kushirikiana na Halmshauri ya Wilaya hiyo.
Sehemu
ya wakulima zaidi ya 100 wa kijiji cha Membe Wilayani Chamwino wakifuatilia
mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kuzalisha kwa tija baada ya kurasimisha
mashamba yao.
(Picha na Frank Mvungi- MAELEZO)
Na; Frank Mvungi, Dodoma
Serikali ya Awamu ya Tano imejikita katika kuwezesha
wananchi kiuchumi kupitia Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za
Wanyonge Tanzania (MKURABITA ) kwa kuwawezesha wananchi kurasimisha ardhi
wanazomiliki yakiwemo mashamba na
kupatiwa hati za kimila za kumiliki ardhi.
Ni vyema wananchi
Wilayanis Chamwino na maeneo mengine ambayo ymeshanufaika na urasimishaji
wakatambua kuwa jukumu lao sasa ni kutumia fursa zitokanazo na urasimishaji kujiletea maendeleo.
Sasa wananchi wote mlionufaika na urasimishaji tambueni kuwa
Serikali imewekeza kwenu kwa kuwajengea uwezo hali inayowawezesha kujikwamua na
kujiletea maendeleo ikiwemo kupata mikopo katika Taasisi za fedha kama mabenki
kupitia hati za kimila za kumiliki ardhi.
Dhamira hii safi ya
Serikali inapaswa kuungwa mkono na wananchi wote ambao wameshanufaika na urasimishaji
uwe wa ardhi au biashara, nalisema hili kwa kuwa nimeshudia hivi karibuni
Mratibu wa MKURABITA Bi Seraphia Mgembe
akihamasisha wananchi wa Wilaya ya Chamwino na maeneo mengine hapa nchini kujitokeza kuchukua hati zao ambazo ni
ukombozi wa kiuchumi na mwarobaini wa umasikini kwa wananchi wanyonge.
Uhamasishaji huu
nimeushuhudia ukifanyika mara kwa mara
na hata wakati wa ufunguzi wa mafunzo
kwa wakulima zaidi ya 100 na viongozi 10 wa Kijiji cha Membe, Wilayani Chamwino
Bi Mgembe alionekana kuguswa na suala la wananchi kuchelewa kuchukua hati zao
za kimila baada kurasimishiwa mashamba yao, akionesha shauku yake ya kutaka
kuona wananchi wanajikwamua kiuchumi kupitia hati hizo.
Kutokana na
urasimishaji huo ambao umefanyika katika Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma jumla ya mashamba 1145 yalipimwa katika Kijiji
cha Membe ambapo hatimiliki 1000 zimeweza kuandaliwa na sehemu
kubwa ya hati hizo hazijachukuliwa na wananchi na kuzitumia katika suala zima la kujenga uchumi na kupanua wigo wa uzalishaji wa mazao
mbalimbali ikiwemo alizeti.
Dhamira hii njema ya Serikali inatekelezwa na Ofisi ya Rais- MKURABITA ambayo imejipambanua kwa vitendo
kutokana na kutekeleza dhana yakujenga
uchumi shirikishi au jumuishi unalenga kuwawezesha wananchi kupitia rasilimali
zilizopo katika maeneo yao ikiwemo ardhi.
Hati hizo ziwe chachu
kwa wananchi kujikwamua kiuchumi na kuunga mkono nia hii njema ya Serikali ya kuwaletea maendeleo; katika hili ni wazi kuwa wananchi wa Wilaya ya Chamwino wamepata
ukombozi wa kiuchumi ambapo sasa wanapaswa kuunga mkono juhudi hizi kwa kuchukua hati hizi.
Aidha, jambo jingine
muhimu ni wananchi wote ambao tayari maeneo yao yamepimwa na kupatiwa hati ni
kuongeza bidii katika uzalishaji ili kuendana na dhana ya ujenzi wa viwanda
ambavyo vinategemea malighafi kutoka katika sekta ya kilimo.
Aidha, faida za urasimishaji ni kama ; kuhakikisha
usalama wa milki kwa kuiongezea thamani
ardhi husika, Kuweza kujipatia mikopo na kuwawezesha wamiliki kuingia ubia
katika uwekezaji kwenye ardhi na kilimo kupitia wadau mbalimbali.
MKURABITA imekuwa
mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa dhamira ya Serikali kuwezesha wananchi
kiuchumi inatimia kwa wakati kutokana na mkazo inaouweka katika kuwezesha
wananchi kurasimisha mashamba yao, viwanja na biashara zao katika maeneo
mbalimbali yaliyofikiwa na mpango huu.
No comments:
Post a Comment