Habari za Punde


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


                   WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Jengo la LAPF
Ghorofa ya Nane,
S. L. P. 25,
Makole Uhindini,
40481 DODOMA.

 
      Coat_of_arms_of_Tanzania
                      TAARIFA KWA UMMA


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mtangazaji Mahiri wa Clouds Media Group, Bw. Ephraim Samson Kibonde kilichotokea jana Jijini Mwanza.

“Msiba huu ni pigo kubwa  kwetu wanatasnia wa habari nchini, tupo pamoja na  wenzetu wa Clouds Media Group katika kipindi hiki kigumu cha majonzi" amesema Dkt. Mwakyembe.

Enzi za uhai wake Marehemu Kibonde alikuwa Mtangazaji wa Redio ya Clouds Fm katika kipindi cha Jahazi, pia alijihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii zikiwemo uandaaji wa  vipindi vya kuelimisha Umma katika masuala ya Makazi na Afya.

Dkt. Mwakyembe ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki, uongozi na wafanyakazi wote wa Clouds Media Group pamoja na wadau wa habari nchini.

Imetolewa na
Lorietha Laurence
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
08/03/2019

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.