Kaimu
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uhandisi na Huduma za Ufundi wa Mamlaka ya
Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Mbila Mdemu (kushoto), jana akimkabidhi
Katibu wa Madrasat-ul-Istiqama, Ustaadh Hemed Suleiman misahafu 29, kwa
niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa wa Mamlaka hiyo, Richard Mayongela.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege Tanzania (TAA), wakishughudia Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Uhandisi na
Huduma za Ufundi, Mhandisi Mbila Mdemu (kushoto) akikabidhi Katibu wa Madrasa
ya Istiqama ya Buguruni, Ghana, Ustaadh Hemed Suleiman moja ya misahafu 29
waliyotoa msaada jana.
Na
Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), jana imetoa
vitabu vya dini aina ya misahafu 29 kwa Madrasat-ul-Istiqama ya Buguruni, Mtaa
wa Ghana, kwa ajili ya watoto wanaosoma elimu ya dini ya Kiislam.
Akikabidhi
vitabu hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Kaimu Mkurugenzi wa Uhandisi
na Huduma za Ufundi, Mhandisi Mbila Mdemu amesema mbali na kazi za kuendesha,
kusimamia na kuendeleza Viwanja vya Ndege Tanzania Bara, TAA imekuwa ikishirikiana
na jamii katika masuala mbalimbali yanayohusu jamii.
Mhandisi
Mdemu amesema pamoja na kwamba Madrasat hiyo ina watoto takribani 230, lakini
anaamini wataweza kupokezana vitabu hivi na kupata mafunzo yaliyo sahihi,
yatakayowajengea malezi bora yenye msingi wa amani na mshikamano.
Amesema
msaada huu wa vitabu vya dini utasaidia kuanza kuwaandaa watoto hao, ambao
baadaye wakiwa wakubwa wanakuwa ni sehemu ya jumuiya na sehemu ya Mamlaka na jamii
nzima ya Kitanzania, ambapo watakuwa waadilifu na wenye maadili mema kwa taifa kwa
kuwa wamepata msingi mzuri wa elimu ya dini, ambao ndio chimbuko la uadilifu na
amani.
“Hii
ni kawaida ya Mamlaka kutoa misaada kwa jamii, na ninaamini msaada huu pia
utasaidia kufanya kitu kikubwa katika jamii yetu, kwa kuwa watoto hawa ndio
watakuja kuwa watumishi wa miaka ijayo, hivyo watakuwa mfano wa kuigwa katika
jamii,” amesema Mhandisi Mdemu.
Pia
Mhandisi, amewakaribisha kutembelea TAA kwa ajili ya kujifunza na kuwa na ari
ya kufanya kazi na Taasisi hii, ambayo ipo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi).
Naye
Katibu wa Madrasat hiyo, Hemed Suleiman ameishukuru TAA kwa kujitoa kwao kwa
kutoa msaada huo, ambao ni moja ya vitu muhimu kwao.
“Nawashukuru
sana tena sana kwa msaada huu, hatuna cha kuwalipa ila Mungu awazidishie pale
mlipotoa, muendelee kuwasaidia watu zaidi ya sisi” ameshukuru Bw. Suleiman.
No comments:
Post a Comment