Habari za Punde

Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Afanya Ziara Kambi ya Maradhi ya Macho Kwa Watotio Hospital ya Mnazi Mmoja leo.

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akizungumza na Muandishi wa Habari kuhusiana na ziara alioifanya katika kambi ya Macho kwa Watoto,katika Hospitali ya Mnazi Mmoja mjini Unguja kwa kushirikiana na Hospitali ya CCBRT ya Tanzania Bara.

Wizara ya Afya Zanzibar kwa kushirikiana na Hospitali ya CCBRT ya Dar esd salaam wamewafanyia uchunguzi wa macho Watoto 165 katika kambi ya Macho Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.

Kati ya Watoto hao wawili wameonekana kuwa na Kensa ya Jicho na wanatarajiwa kusafirishwa kwenda Tanzania bara kwa ajili ya kufanyiwa matibabu

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed ametembelea kambi hiyo na amesema lengo kuu la ziara hio ni kuangalia namna ya zoezi la Uchunguzi linavyofanyika .

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara hiyo, Waziri wa Afya amesema wizara yake itatoa ushirikiano ili kuhakikisha watoto wote watakaogundulikana kuwa matatizo ya macho wanapata matibabu mapema ili kuwanusu na kupata upofu watakapo kuwa watu wazima.

Alisema hadi sasa maradhi ya macho yaliyogundulika kuwasumbua watoto waliofanyiwa uchunguzi kuwa ni Mtoto wa Jicho, Uvimbe katika macho, Presha ya macho na Uoni hafifu.

Kambi hiyo ya macho kwa watoto itadumu kwa wiki moja na Waziri Hamad Rashid amewaomba wazazi na walezi ambao watoto wao wanamatatizo ya macho kuwapeleka Hospitali kuu ya Mnazimmoja Kitengo cha macho ili kufanyiwa uchunguzi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.