RAYA HAMAD –WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
Watendaji wa Mahakama wametakiwa
kutoa mashirikiano na taasisi ambazo zipo nje ya Mahakama ikiwemo Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka , Jeshi la
Polisi ili ufatiliaji na muendelezo wa kesi ziweze kukamilika kwa wakati
Iwapo hakutakuwa na mashirikiano ni wazi
kuwa mianya ya Rushwa na ukiukwaji wa maadili hautakuwepo jambo ambalo haliwezi
kuleta ufanisi na hivyo kupelekea malalamiko ya wananchi ambao wanahitaji huduma
za mahakama hasa katika kupata ufumbuzi wa kesi zao
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Khamis Juma
Mwalim ameyasema hayo alipokutana na watendaji wakuu Mahakama wakiwemo Majaji
na Mahakimu pamoja na Makadhi wa Mikoa
miwili ya Pemba ambapo amewataka watendaji hao kutambua na kuelewa kuwa rushwa ni
adui anaeuwa na kuhujumu uchumi wanchi hivyo hawapaswi kuikaribia iwe
kutoa ama kupokea
Amewataka Majaji kuongeza kasi na uwezo wa kusikiliza kesi na kutoa maamuzi
sahihi kwa haraka na wakati pasina
kuingizwa sitofahamu ama kuingiza masuala yasiyoendana na maadili ya kazi na kutolea mfano wa kesi za
Ubakaji na udhalilishaji kuhakikisha wanatoa adhabu kwa mujibu wa taratibu za
sheria zilizopo ili yeyote mwenye tabia hii chafu aogope na asitamani kufanya
kosa la udhalilishaji na kusisitiza kuwa wadhalilishaji ni watu makatili wasio na huruma hivyo
hawastahilki kuonewa huruma
Waziri Khamis pia amewakumbusha Watendaji hao kuwa uwepo wa
Taasisi ya Mahakama ni utekelezeji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi hivyo ni
vyema kuitumikia wananchi kuitekeleza kwa vitendo kwa maslahi na maendeleo ya
nchi
Ameahidi kuendelea kushughulikia suala la
uhaba wa nafasi pamoja stahiki zao
ambapo taayari Serikali kuu
inatambua tatizo hilo pamoja na kuwataka Watendaji kutoridhika na kiwango cha
elimu walichonacho pamoja na kutoa elimu kwa jamii kutokwepa kutoa ushahidi ili Kesi ili waweze kuisaidia
mahakama
Katibu Mkuu wa Wizara hio ndugu George Kazi
amesema jukumu la usimamizi wa Katiba na Sheria ndilo walilokabidhiwa ambapo
ndani yake zinapatikana taasisi za Mwanasheria Mkuu, Mahakama, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, Ofisi ya Mufti na
Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana hivyo itakuwa si sahihi kuona taasisi hizi
zinakiuka maadili
Sheria ya usimamizi wa Mahakama inatakiwa
ifuatwe sheria ambayo imegawanya majukumu ya kiutendaji na kiutawala ili
masuala ya Mahakama yasiingiliane yatekelezwe na mujibu wa taratibu hivyo
sheria inapofuatwa hakutakuwa na mrundikano wa kesi na ndio maana Wizara baada
kuona umuhimu ilitoa vitabu vingi kwa kila hakimu ili vifanyiwe kazi na kuelewa
wajibu wao
Aidha aliwasisitiza viongozi wa Mahakama
kushirikiana na Wizara ili Waziri aweze
kusimamia vyema na kufahamu masuala yote ya muhimu kwa maslahi na maendeleo ya
wizara hasa suala la uwekaji wa takwimu
sahihi ambazo zitasaidia kuwepo kwa uhalisia sio wa kupikwa na utaratibu mzuri
ili kuwa na kumbukumbu nzuri za kiutendaji “ Waziri ndie anaekwenda kujibu
masuala katika chombo cha kutunga sheria tuwe karibu nae na kufikisha taarifa
kwa wakati tusisubiri mpaka tuhimizwe bali tufahamu wajibu wetu ”
Nae Mtendaji Mkuu wa Mahakama ndugu Kai
Bashiru amesema Wizara inafahamu kuwa Mahakama inakabiliwa na baadhi ya
changamoto lakini mashirikiano ya Wizara
na watendaji yataweza kutatua changamoto
hizo kiufanisi
Katika utekelezaji wa sheria ya Utawala wa Mahakama Idara imejipanga kutekeleza na
kusimamia muundo wa watendaji , majukumu ya wafanyakazi, kufanya tathmini kwa
watendaji ili kuleta ufanisi hatua
ambayo itawezesha pia kuwapima watendaji utendaji wao wa kazi kuanzia Majaji na
Mahakimu ili kufahamu wapi kesi zimekwama na kwanini ikiwemo kupata takwimu
sahihi ya kesi zinazohukumiwa pamoja na
kusisitiza ufinyu wa bajeti inakuwa ni
kikwazo lakini watahakikisha wanayapa kipaumbele kwa kuyasimamia vyema maslahi
ya wafanyakazi wote ili kujenga ari ya kutendaji
Akitoa taarifa fupi Naibu Mrajis wa
Mahakama Kuu na Mrajis wa Jimbo Mahakama Kuu Pemba Mhe Abdulkadir Ali amesema Pemba ina jumla ya
wafanyakazi 120 wanawake 41 na wanaume 79 idadi ambayo inajumuisha kada ya
Mahakimu na Makadhi
Katika kila kituo cha kuna Mahakama ya Kadhi zinazoshughulikia
masuali ya Kiislam kama ilivyoongoza sheria ya Mahakama ya Kadhi sheria No. 9
ya mwaka 2017
Malengo makuu ya Mahakama ni
kusikiliza mashauri na kuyatolea maamuzi
kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa na sheria ambapo Mahakama ya Pemba
inajumuisha vituo vikuu vitano ikiwemo Mahakama kuu Chake chake , Mahakama ya
Wilaya Mkoani, Mahakama ya Mwanzo Kengeja, Mahakama ya Mkoa Wete na Mahakama ya Wilaya
Konde
Mkurugenzi wa Wizara hio ndugu Juma Ali
Simai amesisitiza suala la nidhamu heshima na uwajibikaji na kusema kuwa
linamhusu kila mfanyakazi kufanya hivyo kutasaidia kuondosha mapungufu nakasoro
ziliopo katika ngazi zote na hivyo kutoa huduma bila ya upendeleo .
Akitoa shukurani kwa niaba Taasi ya
Mahakama Pemba Hakimu wa Mkoa Kusini Pemba Mhe Luciano Makoye Nyengo kuhusu
mrundikano wa baadhi ya kesi amesema
sheria ipo wazi na kutolea mfano iwapo kesi miezi mine haijasikilizwa
kisheria ifutwe ingawa jamii hawezi kuelewa na hapo ndipo panapotokea
sitafahamu kwa jamii
Pia ameziomba taasisi ambazo wanafanya nao
kazi kwa karibu kujitahidi kusimamia na kufatilia kutatua baadhi ya mkigogoro
ya kesi kabla kufikisha mahakamani kwani
sio lazima kila kesi hufikishwa mahakamani zipo kesi ambazo kuna taratibu
zikifutwa zinawezwa kumalizwa kwa ngazi ya chini badala kuzifikisha mahakani na
kusababisha kuwepo kwa mlolongo wa kesi .
Luciano ameiomba Wizara kuandaa makaazi
maalum ya Mahakimu na Majaji wa Mahakama
ili wawe huru na kazi zao kwa vile kulingana
na mazingira yao ya kazi si rafiki
sehemu wanazoishi za uraiani ni tatizo kesi wanaziamua ni nzito hivyo
wanahitaji kuishi maeneo salama zaidi
No comments:
Post a Comment