Habari za Punde

Walimu wa Sayansi Kutoka Nchini Nigeria Wawasili Kisiwani Pemba.


Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Ndugu Moh’d Nassor Salim akizungumza na ujumbe kutoka Shirika la kujitolea la Nigeria-Technical Aid Corps (TAC) katika Ukumbi wa ofisi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Chake chake Pemba.
Ujumbe kutoka Shirika la kujitolea la Nigeria-Technical Aid Corps (TAC). (Kulia) niAdamu Jibirillaambae ni Mkuu wa Ufuatiliaji na Tathmini na (kushoto) ni Hammawa Bunuyaminu Ofisa wa Mradi.
Walimu wanaojitolea kutoka Nchini Naigeria wakiwa katika Ukumbi wa ofisi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Chake chake Pemba.

Na Ali Othman Ali
Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Ndugu Moh’d Nassor Salim amesema kupanda kwa kiwango cha ufaulu Kisiwani Pemba kumechangiwa na juhudi zinazofanywa na  Shirika la kujitolea la Nigeria kwa kuleta walimu wa Masomo ya Sayansi.

Akizungumza na ujumbe kutoka Shirika la kujitolea la Nigeria-Technical Aid Corps (TAC) pamoja na walimu 16 wanaojitolea kutoka Nchini Naigeria katika Ukumbi wa ofisiya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Chake chake Pemba Bw. Salim amesema kiwango cha ufaulu Kisiwani Pemba kimepanda kwa asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Mkuu wa Shirika la Kujitolea la Nigeria Bw. Adamu Jibirilla akielezea shukran zake za dhati kwa uongozi wa Wizara ya Elimu kwa mashirikiano makubwa waliyoyapata amewataka walimu hao kundelea kufanya kazi kwa bidii na kuwatabahisha kwamba huduma zao ni zenye kukubalika kisiwani Pemba.

Aidha Bw. Jibirillaamewataka walimu hao kuitumia vyeme fursa ya kuwepo kisiwani Pemba kwa kujifunza lugha ya Kiswahili ambayo ameitaja kua ni lugha inayozidi kujipatia umaarufu katika bara la Afika na Ulimwenguni kote.

Kwaupande wao walimu hao wakujitolea walipata fursa ya kuelezea mafanikio na changamoto mbali mbali zinazowakabili, ambapo mwalimu Yahaya Otori Muhammed anaefundisha Skuli ya Utaani ameliomba Shirika la kujitolea la Nigeria-Technical Aid Corps (TAC) kukubali maombi ya kuleta walimu wengine kujitolea katika Skuli za Zanzibar.

Nae mwalimu Bernard Augbedion anaejitolea katika Skuli ya Ukunjwi, alimuomba Mkuu wa Shirika la hilo Bw. Adamu Jibirilla, kuzingatia swala la jinsia wanapoleta walimu kisiwani Pemba ambapo alisema kwenye mwanaume mwenye mafanikio lazima kuna mwanamke nyuma yake.

Jumla ya walimu 16 kutoka Nigeria (wote wanaume) wanafundisha Skuli mbali mbali za Sekondari kisiwani Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.