Habari za Punde

Mrajisi wa Vyama Vya Michezo Zanzibar Azungumza na Waandishiu wa Habari Kuhusiana na Marekebisho ya Katiba Mpya ya ZFF


Na,Hawa Abdallah. Zanzibar.
MRAJISI wa Vyama vya Michezo Zanzibar Suleiman Pandu Kweleza amesemamabadiliko yaliyofanyika ndani ya ZFA kutoka chama hadi shirikisho yana nia ya kuhakikisha kwamba soka la Zanzibar linakuwa na linasimamiwa kwa misingi ya kimataifa.

Hayo aliyaeleza mbele ya waandishi wa habari  Kuhusu muktaza mzima  wa mabadiliko ya  katiba ya ZFA na ambayo ilikuwaki yanaendeshwa  kwa ajiliya kusimama mpira hapa Zanzibar na kuwa Shirikisho la Soka Zanzibar ZFF ambalo itakuwa na nia na misingi ya kuweza kusimamia soka laZanzibar.

Alisema   tayari katiba hiyo imesharasimishwa na ofisi ya Mrajisi ili iweze kutumika na kwamba maeneo ambayo yamebadilika ni kama ambavyo waliona ni suala zima la chama chenyewe.

“Na naomba mufahamu kwamba mabadiliko haya yaliyofanyika inaonekana kwamba yalikuwa na nia ya kuhakikisha kwamba soka la Zanzibar linakuwa na linasimamiwa kwa misingi ambayo mashirikisho ya kimataifayanaelekeza”, alisema.

Akifafanua  baadhi ya vifungu ambavyo vimebadilishwa katika katiba hiyo alisema kuwa katiba iliyopita ilikuwa inatambuwa uongozi wake kwa kuwa na rais na makamo wawili ambao walikuwa wanaongoza hii ZFA lakini kwenye mabadiliko haya suala hilo limeachwa na kilichofanywa ni Shirikisho ambalo  litakuwa na makamo mmoja ambae yeye ndie atakaemsaidia rais  katika kutekeleza shughuli zake.

Hivyo alisema kuwa  ukiangalia maeneo hayao kile kipengele ambacho kinasomeka kwamba kutakuwa na makamo wawili  mmoja Pemba na mmoja Unguja kimeondolewa na badala yake rais na makamo wake watashirikiana na kusimamia shirikisho hilo kwa pamoja.

Aidha alisema kuwa Katiba ya nyuma ilikuwa inatambuwa uwepo wa kamati tendaji isiyopunguwa watu 31 ambapo kwa upande wa Unguja walikuwa 17 na Pemba 14 kitu ambacho kilionekana kilikuwa kinakwaza kunako maamuzi kwa maana ya kwamba upande wa Unguja au Pemba  kamati ilikuwa nafursa au uwezo wa kutoa maamuzi ya jambo lolote linalokuwa linahusumaendeleo au linahusu mchakato wa mazingira yoyote ya kusimamia sokala Zanzibar kitu ambacho kwa njia moja au nyengine kilikuwa kinalalamikiwa sana

“Nikiwa shahidi wa hilo kama mrajisi nilipata malalamiko mengi ambayo yalikuwa yanatolewa maamuzi, mambo mengi yalikuwa yanakwaza upande mwengine lakini kwa kweli katiba ilikuwa inaamrisha hilo na ilikuwa nishida kuyatatua mambo hayo”, alisema.

Hivyo alisema kuwa  Shirikisho hilo au mabadiliko haya ambayo yamekujasasa hivi inaonekana kwamba kipengele kile kimetoka na badala yake kwamba kamati tendaji ya ZFF ambayo ndio itakayokuwa kamati tekelezaji itakuwa ipo moja ambayo ndio itakayokuwa inasimamia  soka Zanzibar nzima

Kuhusu nafasi mbili za uteuzi wa rais katika katiba alisema kuwa ,Katiba iliyopita rais alikuwa na uwezo wa kuchaguwa wajumbe wawili kuwaingiza katika kamati tendaji kipengele hichi kimehusishwa lakini kimemtaka rais baada ya kuchaguwa wajumbe hao wawili  ni kuweza kuwachaguwa watu ambao wanaonekana wanaweza kusaidia kutekeleza shughuli hizi  za michezo na pia azingatie na maoni ya kamati tekelezaji.

Hata hivyo aliwataka waandishi pamoja na wadau kufika katika ofisi za ZFF kwa ajili ya kuweza kutafuta katiba hiyo ili kuondokana na malalamiko juu ya utekelezaji wa shirikisho hilo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.