MenejaKiongozi ,
UhusianoMfukowaHifadhiyaJamiikwaWatumishiwaUmma (PSSSF) Eunice
ChiumeakizungumzanawaandishiwahabarileoJijini Dodoma
kuhusuhatuailiyofikiwakatikakulipamalimbikizoyamafaoyaoambapoTakribaniwastaafu 10,000/- wamelipwa.
MenejaKiongozi , UhusianoMfukowaHifadhiyaJamiikwaWatumishiwaUmma
(PSSSF) Eunice
ChiumeakitoawitokwawanachamawamfukohuokuendeleakujitokezakatikaOfisizamfukohuokuhakikitaarifazaoiliwawezekuendeleakupatahudumakwamujibuwasheriakuepukausumbufuunaowezaukajitokeza
Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na Meneja Kiongozi
, Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Eunice
Chiume baada yamkutanonawaandishi ha oleo Jijini Dodoma.
Na. Frank Mvungi- MAELEZO
Wanachama elfu kumi wa
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) wamelipwa takribani Bilioni
880, 000/- ikiwa ni malimbikizo ya Pensheni kwa wastaafu tangu kuanzishwa kwa Mfuko huo mapema mwaka
jana.
Akizungumza na
waandishi wa habari leo Jijini Dodoma Meneja Kiongozi, Uhusiano wa mfuko huo Bi. Eunice Chiume amesema kuwa
dhamira ya Mfuko huo ni kuhakikisha kuwa
wanachama wake wanaendelea kulipwa mafao yao kwa wakati kuendana na azma ya
Serikali ya Awamu ya Tano kuwafanya wastaafu wote kuishi maisha bora.
“Katika kipindi cha
miezi 6 Mfuko umeendelea kutoa huduma bora hali iliyowezesha wastaafu wetu zaidi124,000
kuendelea kupata huduma zetu katika ofisi zetu za mikoani pamoja na Zanzibar” alisisitiza
Chiume.
Akifafanua amesema
kuwa mfuko huo una wanachama takribani 763,000 kote nchini na unaendelea
kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma bora kwa wanachama wake.
Mfuko huo umeendelea
kutekeleza dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kusimamia uwekezaji katika
sekta hiyo ikiwemo kiwanda cha viatu Karanga kilichopo Moshi Mkoani Kilimanjaro kinachomilikiwa kwa ubia
na Jeshi la Magereza.
Eneo jingine ni
uwekezaji katika amana za Serikali, kiwanda cha Tangawizi kilichopo Same Mkoani
Kilimanjaro.
Kwa upande wa zoezi
la uhakiki wa wanachama wa mfuko huo amesema kuwa zoezi hilo limefanyika kati
ya Desemba 2018 hadi Machi 2019 na ni endelevu.
Pia alitoa wito kwa
wanachama wa mfuko huo ambao wamestaafu kuhakiki taarifa zao kupitia ofisi za
mfuko huo zilizopo mikoani ili kuepuka usumbufu ikiwemo kusitishiwa pensheni.
Aliongeza kuwa
dhamira ya kufanya uhakiki huo ni kuwezesha mfuko kuhakikisha kuwa anayelipwa
pensheni ni yule anayestahili kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo.
Kwa upande wa
watumishi wa mfuko huo wameaswa kuendelea kutoa huduma bora kwa wanachama wa
mfuko huo ili kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inayosisitiza utoaji
wa huduma bora.
Mfuko wa PSSSF ni
matokeo ya kuunganishwa kwa mifuko ya PSPF, LAPF, GEPF na PPF ili kuimarisha
utoaji wa huduma kwa wananchi hasa kuchochea ukuaji wa sekta ya hifadhi ya
Jamii hapa nchini.
No comments:
Post a Comment