Habari za Punde

PSSSF Yatumia Bilioni 880,000 Kulipa Mafao


 MenejaKiongozi , UhusianoMfukowaHifadhiyaJamiikwaWatumishiwaUmma (PSSSF) Eunice ChiumeakizungumzanawaandishiwahabarileoJijini Dodoma kuhusuhatuailiyofikiwakatikakulipamalimbikizoyamafaoyaoambapoTakribaniwastaafu  10,000/- wamelipwa.


 MenejaKiongozi , UhusianoMfukowaHifadhiyaJamiikwaWatumishiwaUmma (PSSSF) Eunice ChiumeakitoawitokwawanachamawamfukohuokuendeleakujitokezakatikaOfisizamfukohuokuhakikitaarifazaoiliwawezekuendeleakupatahudumakwamujibuwasheriakuepukausumbufuunaowezaukajitokeza
Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na Meneja Kiongozi , Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Eunice Chiume baada yamkutanonawaandishi ha oleo Jijini Dodoma.

(PichazotenaIdarayaHabari MAELEZO)



Na. Frank Mvungi- MAELEZO                                                                                                                 
Wanachama elfu kumi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) wamelipwa takribani Bilioni 880, 000/- ikiwa ni malimbikizo ya Pensheni kwa wastaafu  tangu kuanzishwa kwa Mfuko huo mapema mwaka jana.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma Meneja Kiongozi, Uhusiano  wa mfuko huo Bi. Eunice Chiume amesema kuwa dhamira ya  Mfuko huo ni kuhakikisha kuwa wanachama wake wanaendelea kulipwa mafao yao kwa wakati kuendana na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kuwafanya wastaafu wote kuishi maisha bora.
“Katika kipindi cha miezi 6 Mfuko umeendelea kutoa huduma bora hali iliyowezesha wastaafu wetu zaidi124,000 kuendelea kupata huduma zetu katika ofisi zetu za mikoani pamoja na Zanzibar” alisisitiza Chiume.
Akifafanua amesema kuwa mfuko huo una wanachama takribani 763,000 kote nchini na unaendelea kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma bora kwa wanachama wake.
Mfuko huo umeendelea kutekeleza dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kusimamia uwekezaji katika sekta hiyo ikiwemo kiwanda cha viatu Karanga kilichopo Moshi  Mkoani Kilimanjaro kinachomilikiwa kwa ubia na Jeshi la  Magereza.
Eneo jingine ni uwekezaji katika amana za Serikali, kiwanda cha Tangawizi kilichopo Same Mkoani Kilimanjaro.
Kwa upande wa zoezi la uhakiki wa wanachama wa mfuko huo amesema kuwa zoezi hilo limefanyika kati ya Desemba 2018 hadi Machi 2019 na ni endelevu.
Pia alitoa wito kwa wanachama wa mfuko huo ambao wamestaafu kuhakiki taarifa zao kupitia ofisi za mfuko huo zilizopo mikoani ili kuepuka usumbufu ikiwemo kusitishiwa pensheni.
Aliongeza kuwa dhamira ya kufanya uhakiki huo ni kuwezesha mfuko kuhakikisha kuwa anayelipwa pensheni ni yule anayestahili kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo.
Kwa upande wa watumishi wa mfuko huo wameaswa kuendelea kutoa huduma bora kwa wanachama wa mfuko huo ili kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inayosisitiza utoaji wa huduma bora.
Mfuko wa PSSSF ni matokeo ya kuunganishwa kwa mifuko ya PSPF, LAPF, GEPF na PPF ili kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi hasa kuchochea ukuaji wa sekta ya hifadhi ya Jamii hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.