Kaimu Mkurugenzi Mkuu
wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA, Adam
Fimbo akizungumza na Waandishi wa Habari(hawapo pichani) katika Semina
ya siku mbili ya kuwajengea uwezo
Wahariri na Waandishi wa Habari katika kuelimisha jamii juu ya masuala ya
usalama wa Chakula inayoendelea Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
Kaimu Mkurugenzi wa
Usalama wa chakula wa TFDA Bw. Moses Mbambe, akiwasilisha Maada kuhusu majukumu
ya TFDA katika Semina ya siku mbili ya
kuwajengea uwezo Wahariri na Waandishi wa Habari katika kuelimisha jamii
juu ya masuala ya usalama wa Chakula inayoendelea Wilayani Bagamoyo Mkoani
Pwani.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na
Dawa TFDA, Adam Fimbo, akiwa kwenye
picha ya Pamoja na Waandishi wa Habari, mara baada ya kufungua Semina ya siku mbili ya kuwajengea uwezo Wahariri na
Waandishi wa Habari katika kuelimisha jamii juu ya masuala ya usalama wa
Chakula inayoendelea Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
(Picha na Paschal Dotto-Maelezo )
Na Grace Semfuko,MAELEZO.
Mamlaka ya Chakula na Dawa
Tanzania TFDA imeweka mfumo maalum wa udhibiti wa usalama wa chakula
kinachozalishwa ndani ya nchi na kile
kinachoingizwa kutoka nje ili kuwahakikishia afya bora kwa walaji.
Mfumo huo ni kufanya tathmini ya
vyakula vilivyofungashwa,kusajili maeneo na kutoa vibali vya biashara za
vyakula, kufanya ukaguzi wa vyakula katika soko pamoja na ukaguzi wa maeneo ya
kusindikia, kuhifadhia na kuuzia vyakula.
Akizungumza wakati akifungua
Semina ya siku mbili kwa waandishi wa Habari iliyofanyika Wilayani Bagamoyo
Mkoani Pwani Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Adam Fimbo alisema mfumo huo pia
unalenga kuchunguza sampuli za vyakula katika maabara.
“Ndugu zangu Waandishi wa Habari,
naomba muufahamishe Umma kuwa mfumo huu unahakikisha kila Mtanzania anatumia
chakula salama, na tunaanzia mipakani na kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini”
alisema Fimbo.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Usalama
wa chakula wa TFDA Bw. Moses Mbambe alisema umuhimu wa usalama wa chakula
Nchini Tanzania unapewa kipaumbele kwa kushirikiana na Baraza Kuu la umoja wa
mataifa ambapo kupitia kikao chake cha Desemba 28 2018 ilipitisha siku ya
usalama wa Chakula Duniani kuwa Juni 7 ya kila mwaka ambapo kwa mara ya kwanza
Duniani kote siku hiyo ilianza mwaka huu wa 2019.
“Tanzania tunaungana na Umoja wa
Mataifa katika kuhakikisha tunakuwa na kiwango cha hali ya juu cha usalama wa
chakula,tunawaomba wananchi wazingatie uzalishaji bora wa vyakula na hii itaongeza ufanisi na kuimarisha afya za
wananchi wetu” alisema Mbambe.
Kwa mujibu wa shirika la Afya
Duniani WHO takribani Watu Milioni 600 Duniani sawa na Mtu mmoja kati ya watu
10 huugua kila mwaka kutokana na kula chakula kisicho salama na kati yao watu
420,000 hufariki na huku watoto
wakiwa 125,000 wenye umri wa chini ya
miaka mitano ambapo kwa Bara la Afrika zaidi ya watu milioni 91 wanakadiriwa
kuugua huku watu 137,000 hufariki dunia kila mwaka.
No comments:
Post a Comment