Habari za Punde

Ujumbe wa Taasisi ya Al Hikma Foundation Ukiongozwa na Mwenyekiti Wake Sheikh Nurdin Kishki Wajitambulisha Kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti swa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Katibu wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga akiutambulisha Ujumbe wa Taasisi ya Al-Hikma Foundation ya Jijini Dar es Salaam, walipofika Ikulu Zanzibar leo. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibaer Sheikh. Saleh Omar Kabi, kabla ya kuaza kwa hafla hiyo, kushoto Mwenyekiti wa Taasisi ya Al-Hikma Foundation ya Jijini Dar es Salaam Sheikh Nurdin Kishki na Sheikh Suleiman Khamis Habib, wakiwa katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar waliupofika kijitambulisha leo.   
Mwenyekiti wa Usalama na Itifaki na Mnadhimu Mkuu wa Taasisi ya Al-Hikma Foundation Sheikh. Suleiman Khamid Habib, akizungumza na kuutambulisha Ujumbe wa Taasisi hiyo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, walipofika Ikulu Zanzibar kujitambulisha leo.kulia Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Sheikh Nurdin Kishki. na kushoto Ndg. Mussa Rajan Mushi na Sheikh Omar Hussein Mussa Mwenyekiti wa Al Hikma Foundation Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwenyekiti wa Taasisi ya Al-Hikma ya Jijini Dar es Salaam Sheikh Nurdin Kishki kushoto na Sheikh Suleiman Khamis Habib. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Ujumbe wa Taasisi ya Al Hikma Foundation ya Jijini Dar es Salaam walipofiki Ikulu Zanzibar kujitambulisha kwa Rais wa Zanzibar Dk. Shein, ukiongozwa na Mwenyekiti wake Sheikh Nurdin Kishki. 
Ujumbe wa Taasisi ya Al-Hakim Foundation ya Jijini Dar es Salaam wakiwa katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, hayuko pichani.












No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.