Habari za Punde

Timu ya Mnazi Mkali Yaingia Hatua ya Robo Fainali Michuano ya Kipwida

Na.Mwanajuma Juma.
TIMU ya soka ya Mnazi Mkali imetangulia hatua ya robo ya fainali ya michuano ya kombe 
la Kipwida kufatia ushindi wa mabao 2-0  dhidi ya Kisakasaka.
Mnazi mkali inakuwa timu ya kwanza kutinga hatua hiyo baada ya kufikisha pointi saba 
katika kundi D ambalo linaloundwa na timu za Langasta, Mafriji, Sarayevo Home 
Boys na Kisakasaka ambazo zote zina pointi moja moja.
Katika mchezo huo timu hiyo ambayo imebakisha mchezo mmoja mabao yake yaliwekwa 
kimiyani na wafungaji wake Abdul Hamad dakika ya 78 na Hair Abuu dakika ya 82.
Michuano hiyo leo itaendelea tena kwa kupigwa mchezo wa kundi A ambao utawakutanisha 
Lion Kids na Nyamanzi City.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.