Habari za Punde

Aliyekuwa Kocha wa Timu ya Pamba ya Mwanza Ali Omar Kisasa Amesema Yuko Huru Kuifundisha Timu Yoyote Tanzania Baada ya Kumaliza Mkataba Wake.

Na. Mwanajuma Juma.
ALIEKUWA kocha wa timu ya soka ya Pamba SC Ali Omar Kisaka amesema kuwa 
kwa sasa yupo na yupo tayari kufanya kazi  
na timu yoyote ambayo itamuhitaji baada ya 
kumaliza mkataba na timu hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi 
Kisaka alisema kuwa anashukuru kumaliza 
mkataba na timu hiyo bado hajapokea 
taarifa yoyote kutoka kwa uongozi baada ya 
kumaliza ligi.
Kisaka ambae aliifundisha timu hiyo baada 
aliekuwa kocha wao Juma Sumbu kupata      
maradhi ya kupooza alisema kuwa anashuku
ru kumaliza ligi hiyo na kuibakisha daraja 
ingawa alishindwa kuipandisha na 
kucheza ligi kuu.
“Mpaka sasa nipo, nimemaliza mkataba na sijapokea taarifa yoyote kutoka kwa uongozi 
wangu lakini kama kutatokea timu nipo tayari kufanya nayo kazi”, alisema.
Akizungumzia ligi ya Tanzania Bara alisema kuwa ni ngumu na yenye ushindani sambamba 
na kuwepo kwa vitisho hasa timu inapotoka kwenda kucheza katika mkoa mwengine.
Hata hivyo alisema kuwa kupitia ligi hiyo ameweza kupata mafanikio makubwa ikiwemo 
akili yake kukuwa kielimu zaidi.
“Nimefanya vizuri japo mtu hajioni mwenyewe aneona yupo  juu lakini nimepiga hatua”, 
alisema.
Timu hiyo aliichukuwa ikiwa katika nafasi ya sita pointi 14 ambapo alifanikiwa kuifikisha 
hatua ya kupanda lakini 
lishindikana baada ya kutolewa katika mchezo wa mwisho na timu ya Kagera Sugar na 
kushindwa kupanda.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.