Habari za Punde

Waarabu wa Msuva wamtaka Mudathir Yahya

Klabu ya Difaa Al Jadid ya Morocco ambayo anaichezea Mtanzania, Simon Msuva ina mpango wa kumsajili kiungo wa Azam FC, Mudathir Yahaya.

Kiungo huyo ni mmoja kati ya wachezaji ambao walipeperusha bendera ya Tanzania kwenye michuano ya Afcon ambayo Taifa Stars ilitolewa hatua ya awali kabisa.

Hata hivyo, taarifa zilizopo ni kuwa, Waarabu hao wa Morocco wana mpango wa kutaka kumsajili nyota huyo wa Azam baada ya kuvutiwa na uwezo wake.

Kiungo huyo, Mudathir Yahya, alisema: “Wakati nikiwa kule Misri kwenye michuano ya Afcon, hakuna mtu yeyote aliyenifuata kuhusu dili hilo, lakini kama lipo, nipo tayari kuondoka.”

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.