RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amemteuwa Dkt. Zakia Mohammed
Abubakar kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar katika Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali.
Dkt. Zakia anachukuwa nafasi iliyowachwa wazi na Profesa Idris
Ahmada Rai ambae anamaliza muda wake wa kutumikia wadhifa huo kwa mujibu wa
sheria.
Uteuzi wa Dkt Zakia umefanyika kwa mujibu wa uwezo aliopewa
Rais, chini ya kifungu cha 9 (1) cha Sheria ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar,
namba 8 ya mwaka 1999.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyosainiwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Abdulhamid Yahya Mzee,uteuzi huo utaanzia Septemba, 06, mwaka huu.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment