Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanznaia, Dkt. Bernad
Kibese( wa pili kulia) akimuonesha Gavana wa
Benki Kuu ya Tanzania , Prof. Florence Luoga ( wa tatu kulia), mara
baada ya Mkutano na waandishi wa habari ulifanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu
Jijini Dar es Salaam, Disemba 17, 2019, wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Hai (wa
kwanza kulia) na viongozi kutoka BOT.
Na.Mwandishi Wetu-MAELEZO.
Serikali imesema itaandelea kufanya oparesheni ya
uhujumu uchumi ili kudhibiti utengenezaji na upatikanaji wa fedha bandia katika
maeneno mengi nchini na itahakikisha kuwa inatoa elimu juu ya madhara ya
uingizwaji wa fedha bandia katika mzunguko fedha hizo.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari,
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florence Luoga amsema kuwa mwananchi
yeyote afanyae kazi ya kutengeneza au kumiliki fedha bandia ni kosa la jinai na
akibainika sheria itachukua mkondo wake.
“kupatikana na noti bandia ni kosa ambalo halihitaji
ushahidi, maana wewe unayepatikana na noti au fedha haramu baada ya hapo
unapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria na ufungwe, kwa hiyo wakati wa elimu ya
noti bandia inatolewa nawatahadharisha wananchi wanatakiwa kuhakikisha
hawapatikani na noti au fedha haramu”, Alisema Prof. Luoga.
Prof.Luoga aliwataka wananchi wanaotamani kujiingiza
kwenye uhujumu uchumi wa kutengeneza fedha bandia wajiepushe kabisa kujiingiza
huko kwa kuwa Benki Kuu na vyombo vya dola sasa vipo kwenye mapambano ya
uhujumu uchumi.
Alisema kuwa wahujumu uchumi wanaweza wakaharibu
uchumi kwa kuchagiza mfumuko wa bei kuwa kuingiza fedha haramu katika mzunguko
wa fedha za nchi hali ambayo inamadhara makubwa sana kiuchumi.
Aidha aliwapongeza vyombo vya dola kwa kushirikiana
katika mapambano ya kuondoa fedha bandia katika mzunguko wa uchumi kwa kukamata
waharifu wanajihusisha na utengenezaji wa fedha bandia kule Chanika Jijini Dar
es Salaam, aliongeza kuwa Benki Kuu ina fedha za kutosha za kigeni ambazo
zinaweza endesha uchumi bila shida yoyote.
“Sasa hivi nchi yetu ina fedha za kutosha za kigeni
hata yale mazoea ya kutishiwa kuwa nchi haina fedha za kigeni za kutosha kwa
hiyo hatuwezi kuendesha shughuli zetu hilo siyo tatizo kwa sasa kwea nchi yetu kwani
kwa sasa tunapesa za kutosha”, Alisisitiza Prof. Luoga.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar
es Salaam, Lazaro Mambosasa alisema kuwa mnamo Desemba 15 mwaka huu Jeshi la
Polisi lilimkamata mkazi wa Chanika Jijini Dar es Salaam na wenzake wawili
wakijihusisha na uendeshaji wa kiwanda cha kutengeneza noti bandia.
“Jeshi la Polisi na Wadau wengine wa Masuala ya ulinzi
na usalama pamoja na Menejimenti ya BOT tumeweza kuiwakamata waharifu sugu
wanaojihusha na uendeshaji wa kiwanda cha kutenegeneza noti bandia na
tukakamata noti bandia za nchi mbalimbali ambazo wametengeneza”, Alisema
Kamanda Mambosasa.
Mambosasa alisema kuwa oparesheni hii ilianzia
Wilayani Hai baada ya Mkuu wa Wilaya hiyo Lengai Ole Sebaya kukamata noti
bandia Zaidi ya shilingi milioni 11, huku kwa Dar es Salaam zikikamatawa noti
za kitanzania 10,540, dola za marekani 133, 048, Msumbiji noti 110,23, Congo
DRC noti 2,270, Kenya noti 1 pamoja na Malawi noti 1.
No comments:
Post a Comment