Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetiliana saini na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA)Mkataba wa Mkopo wa Dola za Kimarekani Milioni 13.5 kwa ajili ya Ujenzi wa skuli za Sekondari za Ghorofa (Roshani)za Zanzibar.
Sherehe
hizo za utiaji saini mkataba huo wa makubaliano zilifanyika jumamosi 21 Dec
2019 katika Makao Makuu ya Benki hiyo ya BADEA Khartoum nchini Sudan, ambapo
kwa Upande wa Tanzania mkataba huo umesainiwa na Mheshimiwa Mohammed Ramia
Abdiwawa Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwa upande wa
BADEA umesainiwa na Dkt.Sidi Ould Tah.
Katika
Mradi wa Ujenzi wa Skuli hizo za sekondari Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
itatoa Dola Milioni 1.5 katika kufanikisha.
Skuli
hizo tatu za kisasa zitajengwa katika Mkoa wa Mjini Magharibi,Mkoa wa Kaskazini
Pemba na Mkoa wa Kaskazini Unguja na kufanya jumla ya Skuli za Sekondari
zilizojengwa kwa mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na
Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) kufikia tano,ambapo tayari
skuli mbili zimeshajengwa na moja inatoa huduma Skuli ya Mohammed Juma Pindua
ya Mkoa wa Kusini Pemba na ile ya Sekondari Kibuteni ambayo inatarajiwa
kukamilika ifikapo mwezi Machi Mwaka 2020.
Sherehe
hizo za utiaji saini zimehudhuriwa pia na Balozi wa Tanzania nchini Sudan
Balozi Silima Haji, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Abdulla Mzee Abdulla, Kamishna wa Fedha za Nje katika Wizara ya Fedha na
Mipango Bihindi Nassor Khatib na Loveness Msechu na Ndugu Issaya kutoka Wizara
ya Fedha na Mipango ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
No comments:
Post a Comment