SHIRIKA
la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Dawa za Kulevya na Uhalifu
(UNODC) kupitia kamisheni ya Kimataifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya limeipongeza
Tanzania kwa jitihada madhubuti za kudhibiti na kupambana na tatizo la dawa za
kulevya.
Kwa
mujibu wa taarifa inasema, juhudi hizo zimeleta matokeo chanya katika mapambano ya
dawa za kulevya duniani katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka 2018 hadi
2020.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Kamishna Generali wa Mamlaka ya
Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, James Kaji wakati wa mkutano wake na
Waandishi wa Vyombo vya Habari kuelezea mafanikio makubwa yaliyopatikana nchini
katika kupambana na kudhibiti dawa za kulevya.
“Katika
mkutano wa 63 wa Kamisheni ya Kudhibiti Dawa za Kulevya Duniani (CND 63) uliofanyika
Nchini Austria, ni Mkuu wa shirika la UNODC alitupongeza Tanzania kuwa ni moja
kati ya nchi chache barani Afrika zilizofanikiwa kupunguza upatikanaji na
uhitaji wa dawa za kulevya, na kuweza kutekeleza mikakati minne ya kupambana na
tatizo la dawa za kulevya kwa uwiano ulio sawa“ alisema Kamishna Haji.
Alisema
mafaniko hayo yamekuja kutokana na juhudi za serikali ya Tanzania katika
kufanya marekebisho makubwa ya kisheria, ikiwemo kutungwa kwa Sheria Na. 5 ya Kudhibiti
na Kupambana na Dawa za Kulevya ya mwaka 2015 na mabadiliko yake ya mwaka 2017
kwa Tanzania bara, na kwa upande wa Zanzibar
ambako mabadiliko ya sheria yalifanyika mwaka 2019.
Aidha
Kamishna Haji aliwataka waandishi wa
habari kutoa taarifa za uhakika juu ya takwimu za kupambana na kudhibiti dawa
za kulevya nchini, kwani pasipo kufanya
hivyo kwa kutoa takwimu za uongo kutasabisha hofu na taharuki katika jamii na
kuchafua taswira ya Tanzania.
“Pamoja
na mafanikio hayo makubwa, bado tuna masikitiko makubwa kwa baadhi ya magazeti
wanaichafua nchi yetu kwa kuandika habari zisizo sahihi kuhusu udhibiti na
mapambano dhidi ya dawa za kulevya niwaombe kuwa makini katika uandishi wa
habari na ni vyema kutumia vyanzo vya uhakika na kuzingatia maadili ya
Uandishi” alisema Kamishna Haji
Baadhi
ya Mgazeti hayo ni pamoja na gazeti la The East African la Nchini Kenya katika
toleo lake Na. 1323 la tarehe 07-13 Nachi 2020 na gazeti la Kimtandao la The
Citizen la Tarehe 8 Machi 2020 yaliandika
Tanzania ni Kitovu cha Dawa za Kulevya Afrika Mashariki.
Aidha
Kamishna Haji amewataka Watanzania kuendelea kujivunia kwa mafanikio hayo yaliyopatikana
na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya mfano wa kuigwa katika mataifa ya Uganda,
Msumbiji, Ghana, Nigeria na Norway ambazo zilliomba kujifunza mfumo wa utendaji kazi na sheria ya kudhibiti
na kupambana na dawa kulevya ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment