Na
Jaala Makame Haji- ZEC
Makarani
wa Uandikishaji katika Vituo vya Uandikishaji wamesisitizwa kuwa makini na kufuata Sheria, Kanuni na Miongozo ya Uchaguzi
ili kutoa huduma bora wakati zoezi la uandikishaji na uhakiki wa taarifa za
wapiga kura likiendelea katika vituo vya uandikishaji kwa Mikoa ya Unguja.
Mkurugenzi
wa Uchaguzi Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar THABIT IDAROUS FAINA akifungua mafunzo
ya siku moja kwa Makarani wa uandikishaji huko Elimu mbadala alisema matarajio
ya Tume ni kuandikisha idadi kubwa ya wananchi waliokosa fursa hiyo hapo awali
hivyo ni vyema makarani hao kuwa makini pale wanapotekeleza majukumu yao katika
vituo vya uandikishaji.
Alisema
kwa kuwa Tume inadhamira ya Kumuandikisha kila mwenye sifa atakayefika kituoni
kuomba kuandikishwa ama kuhakiki taarifa zake ni vyema makarani hao kufanyakazi
kwa bidi ili kufikisha dhamira hiyo iliyowekwa na Tume ili Wazanzibari
waliowengi wapate kushiriki katika hatua zote za mchakato wa Uchaguzi.
Mkurugenzi
FAINA alisema, Tume imekamilisha kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za
Wapiga Kwa Mikoa yote ya Pemba kazi ambayo ilianza tarehe 30/5/2020 na
31/5/2020 katika Mkoa wa Kaskazini Pemba na kumalizika Mkoa wa Kusini Pemba
tarehe 01/6/2020 na 2/06/2020 bila kutokezea changamoto yoyote ambayo
ingeathiri mfumo mzima wa uandikishaji.
Ndugu,
FAINA alifafanua kuwa, kwa upande wa Unguja Kazi hiyo ya Uandikishaji itaanza
katika Mkoa wa Kaskazini Unguja tarehe 5 na 6/6/2020 na kuendelea Mkoa wa
Kusini Unguja tarehe 7 na 8/6/2020, tarehe 9 na 10/6/2020 Wilaya ya Magharib A
na Wilaya ya Magharibi “B” na itamalizika katika Wilaya ya Mjini tarehe 11 na
12/6/2020
Alisema
kukamilika kwa kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kura ni hatua
muhimu ambayo itaiwezesha Tume kuweka wazi Daftari, kugawa vitambulisho vya
kupigia kura na kukamilisha kazi ya uchaguzi mkuu. 2020
Akiwasilisha
mada katika mafunzo hayo juu ya utaratibu na miongozo ya kazi ya uandikishaji
Mkuu wa Kurugenzi ya Mifumo ya Uchaguzi Tume ya uchaguzi ya Zanzibar MWANAKOMBO
MACHANO ABUU alisema kazi ya uandikishaji itafanyika kwa muda wa siku mbili kwa
kila kituo cha uandikishaji na kuwataka kuzifanyia kazi changamoto
zilizojitokeza katika zoezi la awali.
Baadhi
ya Makarani wa uandikishaji waliahidi kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi
sambamba na kuwataka wananchi wenye sifa za kuwemo katika Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura kutodharau fursa hiyo ambayo itawapa haki ya kushiriki katika
Uchaguzi Mkuu 2020.
No comments:
Post a Comment