Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wananchi wa Pemba katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Mkoani ya ZSSF, baada ya kukamilika ujenzi wake mkubwa, mkutano huo umefanyika katika uwanja wa zimamoto Mkoanui Pemba leo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amesema kuwa kazi
kubwa ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo imechaguliwa na wananchi ni
kuwahudumia kwani wao ndio waliyoiweka madarakani.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo huko katika uwanja wa Zimamoto Bandarini, Mkoani Pemba
wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la Msingi afisi za
ZSSF Tibirinzi, Afisi za ZRB Gombani pamoja na kuzindua Hoteli ya Mkoani ambayo
imefanyiwa ukarabati mkubwa.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa kazi ya Serikali ni kuwaletea
maendeleo wananchi na kwa hivi sasa Serikali ya Awamu ya Saba imekuwa ikifanya
hivyo kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuwasogezea huduma muhimu za kimaisha.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa tangu kufanyika kwa Mapinduzi ya Januari 12, 1964 Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ilianza kutekeleza ahadi zilizoahidiwa na Chama Cha ASP.
Alisema kuwa hivi sasa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatekeleza ahadi za Chama Cha Mapinduzi
(CCM) ilizoziahidi katika Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020, ikiwa ni
pamoja na kuwahudumia wananchi.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa kuzinduliwa kwa hoteli ya Mkoani ambayo ni miongoni mwa hoteli za Serikali
zilizojengwa mwanzoni mwa miaka 1970 sambamba na ya Chake Chake na ya Wete
ambazo zilikuwa chini ya Shirika la Utalii Zanzibar ambalo kwa sasa halipo
ilikuwa ni kuwahudumikia wananchi wa ndani na nje ya nchi.
Alisema kuwa hoteli ni
kwa ajili ya watu mbali mbali wakiwemo watalii na wananchi ambao wanapata
huduma za kitalii ambayo hatua hiyo inaimarisha utalii wa andani.
Aidha, Rais Dk. Shein
aliwanasihi wananchi nao kwa upande wao kujenga hoteli kwani tayari ZSSF
imeonesha njia na Serikali imewaamini huku akisisitiza kuwa Makampuni,
Mashirika pamoja na Wajasiriamali nao wana nafasi ya kufanya hivyo.
Alieleza kuwa Serikali
zilizopita za Kikoloni hazikuimarisha sekta ya Kitalii na badala yake Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar imeimarisha kwa kiasi kikubwa sekta hiyo tokea
Mapinduzi ya Januari 12, 1964 na kupelekea kuongezeka kwa hoteli na wageni.
Kwa upande wa hatua za
Serikali za kujenga jengo la Afisi za ZRB Pemba, Rais Dk. Shein alisema kuwa
hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kukusanya kodi kwa ajili ya mapato ya
Zanzibar.
“Tukisema wengine
wanaguna na wagune mpaka wagunuke sisi tunasonga mbele kubwa ninalowaambia
wananchi wa Mkoani wajiandae kupokea wageni....Serikali imeridhika na mimi
mwenyewe nimeridhika”,alisema Dk. Shein.
Aliongeza kuwa ZRB
imefanya kazikubwa na ndio maana uchumi wa Zanzibar umeimarika na hivi sasa
kufikia uchumi wa kati kama ilivyo kwa upande wa Tanzania Bara ambapo hivi sasa
uchumi wa Zanzibar umekwua kwa asilimia 7.
Alisema kuwa hivi sasa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikifanya mamabo yake wenyewe wka
kutegemea fedha zake inazozikusanya.
Pamoja na hayo, Kwa
upande wa afisi za ZSSF zinazojenwga huko Tibirinzi, Rais Dk. Shein alisema
kuwa kjengwa kwa afisi kutasaidia kwa kiasi kikuwba kuwawekea mazingira mazuri
wafanyakazi.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa ZSSF imeweza kuanzisha miradi mbali mbali mikubwa Unguja na Pemba hatua
ambayo imepelekea kukua na kuimarika kwa miji yote ya Zanzibar.
Mapema Rais Dk. Shein
alipokuwa akiweka mawe ya msingi katika Afisi za ZSSF huko Tibirinzi na ZRB
huko Gombani alisema kuwa miradi kadhaa inatarajiwa kuendelezwa na mengine
kuanzwa ukiwemo ujenzi wa uwanja wa ndege wa Pemba.
Katika mkutano huo
huko Mkoani, Waziri wa Fedha na Mipango Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa alieleza
mafanikio yaliopatikana kutoka Mfuko wa ZSSF na kutoa historia ya ujenzi wa
hoteli kisiwani humo.
Balozi Ramia
aliwaondoa wasiwasiw ananchi na kuwaeleza kwamba fedha zao zilizoko katika
Mfuko wa Jamii wa ZSSF ziko salama.
Nae Katibu Mkuu wa
Wizara ya Fedha na Mipango Khamis Mussa alisema kuwa maendeleo yameendelea
kupatikana hapa nchini katika miaka 10 ikiwemo katika uwekezaji wa Ofisi za
Serikali na Taasisi zake.
Alisema kuwa kwa
upande wa hoteli ya Mkoani, hoteli hiyo ilifnguliwa Januari 9, 1974 na kutoa
huduma kwa miaka 1970 hadi 1990 ambapo kutokana na kukosa matunzo yanayopaswa
hoteli ilichakaa na kusita huduma zake.
Alieleza kuwa chini ya
uongozi wa Rais Dk. Shein Baraza la Mapinduzi liliamua kuikabidhi hoteli hiyo
kwa ZSSF kwa lengo la kuifufua na kuiendeleza kiuchumi kama lengo la awali
kuijenga kwake ambapo makabidhiano rasmi yalifanyika Oktoba 19 mwaka 2018.
Alisema kuwa Kampuni
ya ARQES AFRICA ya Dar es Salaam ilibarikiwa kazi za kuandaa mchoro mpya kwa
kuzingatia hali ya jengo lenyewe pamoja na mahitaji ya ZSSF ambapo Kampuni ya
ukandarasi ya BENCHMARK ENGENEERING ilibarikiwa Kandarasi ya kukarabati jengo
na kulikabidhi Julai 4, 2019.
Alisema kuwa ujenzi
huo umezingatia watu wenye ulemavu na mahitaji maalum ikiwemo “lift” ambapo
matengenezo ya jengo hilo yamegharimu jumla ya TZS Bilioni 4 ambayo yalichukua
miezi minane.
Aliongeza kuwa Afisi
za ZSSF zinazojengwa Tibirinzi mbele ya Kiwanja cha Kufurahishia watoto cha
Umoja Kampuni ya ARQES AFRICAN ya Dar es Salaam ndio iliyobarikiwa zabuni ya kuandaa michoro ya jengo hilo la
ghorofa tatu ambapo ujenzi umefanywa na kampuni ya Quality Building Contractors
ya Zanzibar.
Alisema kuwa ujenzi
huo umegharimu TZS bilioni saba na mia tisa na thelathini milioni hadi Juni
30,2020 na jumla ya TZS bilioni mbili na milioni mia mbili na arobaini na tisa
zimeshalipwa sawa na asilimia 28.56 ya malipo yote kwa mradi mzima.
Sambamba na hayo,
jengo la ghorofa nne la ZRB Gombani ambalo mkataba wake ni wa mwaka mmoja na
ulitiwa saini mwezi Disemba 2019 na jengo linatarajiwa kukamilika mwezi Disemba
2020 na gharama za ujenzi ni TZS Bilioni 10.6.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment