Baadhi ya Wafamasia walioshiriki maadhimisho ya siku ya Wafamasia Duniani wakimsikiliza Mkurugenzi Mipango Sera na Utafiti Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar khalid Masoud Wazir (hayupo Pichani) katika ghafla iliyofanyika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Mjini Zanzibar.
Mgeni rasmin Mgeni rasmin Mkurugenzi Mipango Sera na Utafiti Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ndg.Khalid Masoud Waziri Katikati akiwa katika picha ya pamoja na Wafamasia baada ya kumalizika kwa mkutano wa mafunzo .
Picha na Maryam Kidiko - Maelezo Zanzibar.
Na Kijakazi Abdalla Maelezo 26/09/2020
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Maalim Abdullah Mzee amewataka wafamasia kufuata maadili ya kazi zao ili kulinda heshima katika kada yao.
Maalim Abdalla ameeleza hayo katika hotuba yake ya siku ya Wafamasia Duniani iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi Mipango,Sera na Utafiti wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo.
Amesema Wafamasia ni moja kati ya kada muhimu katika sekta ya afya ambayo inahitaji watendaji waaminifu na wenye uadilifu katika kutekeleza kazi zao.
Alisema wafamasia wanamchango mkubwa katika jamii ikiwemo kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya dawa katika kukinga na kutibu maradhi mbalimbali .
Aliweka wazi kuwa wafamasia wanawajibu wa kuhakikisha usalama wa dawa kwa wagonjwa wakati wa usambazaji hadi kumfikia mtumiaji.
Kutokana na umuhimu wa kada ya afya, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara y Elimu amewataka wafamasia, madaktari, wauuguzi na wataalamu wa kada hiyo kushirikiana ili kulinda afya za wananchi.
Amewashauri wafamasia kufikiria njia bora ya kuziendeleza dawa za asili ili kupiga hatua za kimaendeleo kama zilivyo nchi nyengine zikiwemo India na China.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafamasia Zanzibar Bwana Mohammed Kheir amewasisitiza wafamasia kuwa kitu kimoja na kuwa waangalifu katika kutekeleza majukumu yao ili kutoa huduma bora kwa wananchi wenzao.
Siku ya Wafamasia Duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 25/09/2020 ya kila Duniani kote na Kaulimbiu ya mwaka huu ni “Wafamasia na Mabadiliko ya Sekta ya Afya Duniani”.
No comments:
Post a Comment