Habari za Punde

Tasaf Yatowa Mafunzo kwa Waandishi wa Habari

KATIBU Tawala Mkoa wa Tanga Judika Omar katikati, akiwaongoza watendaji mbali mbali kutoka Tasaf makao Makuu na waandishi wa habari, katika kumuombea mwanzilishi wa Tasaf Tanzania Marehemu Rais Mstaafu Benjamini Wilium Mkapa, wakati wa kikao kazi cha kuwajengea uwelewa waandishi wa habari kilichofanyika Halmashauri ya Jiji la Tanga.

MKURUGENZI Mtendaji wa Tasaf Tanzania Ladislaus Mwamanga, akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa kwa waandishi wa habari, kuhusu utekelezaji wa kipindi cha Pili cha awamu ya tatu ya Tasaf, huko katika ukumbi wa halmashauri ya jiji la Tanga.

KATIBU Tawala Mkoa wa Tanga Judika Omar akifungua kikao kazi cha kujenga uelewa kwa waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamua ya Tatu ya Tasaf, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf Ladislaus Mwamanga, kikao hicho kilichofanyika halmashauri ya Jiji la Tanga.

MTAALAMU wa Mawasiliano kutoka Tasaf Zuhura Mdungi, akiwasilisha Madhumuni ya kikao kazi cha kuwajengea uelewa waandishi wa habari kuhusu PSSN II, kikao kilichofanyika halmashauri ya jiji la Tanga.
WAANDISHI wa habari kutoka Pemba, Unguja, Morogoro na Dar Esalam, wakifuatilia ufunguzi wa kikao cha cha kuwajengea uelewa kuhusu utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamua ya Tatu ya Tasaf, kikao hicho kilichofanyika halmashauri ya Jiji la Tanga.
WAANDISHI wa Habari kutoka Unguja, Pemba na Tanga wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji kutoka Tasaf na katibu Tawala Mkoa wa Tanga Judika Omar, mara baada ya kufungulia kwa kikao kazi cha kujenga uelewa kuhusu kipindi cha pili cha awamua ya Tatu ya Tasaf, kikao hicho kilichofanyika halmashauri ya Jiji la Tanga.
(PICHA NA ABDI SULEIMAN, TANGA)  
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.