Habari za Punde

Chuo cha Kiislamu chafanya maonyesho ya utamaduni wa Mzanzibari kwenye vyakula na mavazi

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Kiislamu walioshiriki kwenye maonyesho ya utamaduni wa Mzanzibari kwenye vyakula na mavazi.
Mkuu wa chuo cha Kiislamu Ndugu Bakari Chum Ame akionja baadhi ya vyakula vya Mzanzibar alipokuwa akikagua vyakula hivyo kwenye maonyesho utamaduni wa Mzanzibari kwenye vyakula na mavazi yaliofanyika katika Chuo cha Kiislamu Mazizini.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Kiislamu walioshiriki kwenye maonyesho ya utamaduni wa Mzanzibari kwenye vyakula na mavazi.
Mkuu wa chuo cha Kiislamu Ndugu Bakari Chum Ame akizungumza kwenye maonyesho ya utamaduni wa Mzanzibari kwenye vyakula na mavazi yaliofanyika katika Chuo cha Kiislamu Mazizini.
Mitarawanda ya kiasili ambavyo ni viatu vya mbao vikiakisi utamaduni wa Mzanzibari 
 

Mkuu wa chuo cha Kiislamu, Maalim Bakari Chum Ame  amewataka Wanafunzi wa  Chuo cha Ualimu cha Kiislamu kudumisha Utamaduni wa Mzanzibar ili kulinda mila, sulka na tamaduni za nchi .                               

Hayo ameyasema wakati wa maonesho mafupi yanayo husu utamaduni wa mzanzibari ya vyakula na mavazi ya katika ukumbi wa chuo cha kiislamu  mazizini mjini Unguja. 

Amesema  kuendeleza utamaduni wa mavazi kutaifanya jamii kuwa  na tabia na hulka  Nzuri huku utamaduni wa vyakula vya asili uwafanya  kuepukana na maradhi mbalimbali kwa kula vyakula vya asili.

Aidha amewataka wakufunzi na viongozi wa Wanafunzi hao kuendeleza maonyesho hayo  kwani yatachangia kukitangaza chuo hicho kupanda daraja zaidi na  pia kukuza vipaji vya walimu katika ufundishaji.        

Hata hivyo amewataka  Wanafunzi kujitahidi  zaidi katika masomo yao ili kupata Walimu bora watakao saidia kuongeza ufaulu wa Wanafunzi ili kupata wataalamu bora wa baadae.     

Nae msaidizi mkuu wa utawala Ndugu Mohammed Mwinyi  Ramadhan amesema kumekuwepo changamoto ya mporomoko wa maadili hali inayo sababisha kila mzee na mtoto wake na hivyo kupelekea kutokea vitendo mbalimbali vya udhalilishaji. 

Hivyo amewataka walimu ,Wazazi na Walezi kushirikiana katika malezi ya pamojaa na kulinda tamaduni hizo .  

Nae Mkufunzi wa Walimu wa maandalizi na Msingi chini,  Mwalimu Shamir Kombo Ali amesema lengo la kuandaa maonesho hayo ni kuwafanya walimu kutambua vifaa na vyakula vya asili ilinao waweze kuwafundisha Wanafunzi wao kwa kukuza utamaduni wa nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.