Habari za Punde

Hali ya maradhi ya kisukari inatisha kwa kuwepo ongezeko kubwa la wagonjwa wapya

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa  Mnazimmoja Dkt Ali Salum Ali akielezea ongezeko kubwa la wagonjwa wapya wa maradhi ya kisukari Zanzibar, kwa waandishi wa habari huko katika Maadhimisho ya  Siku ya Kisukari Duniani, huko Ukumbi wa Dodoma Mnazimmoja 
Daktari Bingwa wa Maradhi ya Kisukari Dkt. Faidha Kassim Suleiman akitoa takwimu ya wauguzi walifanyiwa vipimo hivi karibuni na kugundulika baadhi yao wanaviashiria vya maradhi ya kisukari katika Maadhimisho ya Siku ya Kisukari Duniani huko Ukumbi wa Dodoma  Mnazimmoja 
 Meneja wa Maradhi ya Kisukari kutoka Hospitali ya Rufaa Mnazimmoja, Bw. Omar Abdalla Ali (aliesimama) akitoa wito kwa jamii kula vyakula sahihi vyenye matumizi ya mbogamboga  na matunda  pamoja na kufanya mazoezi ya viungo katika Maadhimisho ya Siku ya Kisukari Duniani huko Ukumbi wa Dodoma Mnazimmoja .

Baadhi ya Wataalamu wa maradhi ya kisukari pamoja na waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mnazimmoja Ali Abdalla Ali (katikati) kuhusu vichocheo vya maradhi ya kisukari ambavyo hupata watoto ,vijana pamoja na watu wazima katika Maadhimisho ya Siku ya Kisukari Duniani  huko Ukumbi wa Dodoma Mnazimmoja .

 

PICHA ZOTE NA KHADIJA KHAMIS MAELEZO ZANZIBAR .


Na Khadija Khamis – Maelezo Zanzibar 

 

Mkurugenzi wa Hospitali ya Mnazimmoja Dk.Ali Salum Ali amesema hali ya maradhi ya kisukari inatisha kutokana  na ongezeko kubwa la wagonjwa wapya.

 

Akizungumza katika kilele cha siku ya Kisukari Duniani katika ukumbi wa Hospitali ya Rufaa Mnazimmoja amesema kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wapya wa kisukari 300 kila mwaka hapa Zanzibar kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka 2011 ambapo hivi sasa idadi imekuwa kubwa zaidi .

 

Aliwashauri wananchi kuwa na utamaduni wa kupima afya na kufanya mazowezi  pamoja na kupata mlo kamili ikiwa ni pamoja na mbogamboga kwa wingi matunda na uwanga kidogo .

 

Aidha aliwashauri wananchi wenye maradhi ya kisukari kuacha tabia ya kutumia dawa za miti shamba ambazo hazina viwango na hazijathibitishwa.

 

Daktari Bigwa wa Magonjwa ya Kisukari Dk Faidha Kassim Suleiman amesema ongezeko la watoto wanaogunduliwa na kisukari ni watoto saba hadi kumi kwa mwezi na mtoto mmoja  aligudulika na ugonjwa huo mara baada ya kuzaliwa.

 

Amesema takwimu inaonyesha kwa wauguzi  274 walifanyiwa vipimo hivi karibuni  vinaonyesha  asilimia 63..4 ya wauguzi hao wanauzito mkubwa  3.2 wanaviashiria vya sukari, 10.2 wanapresha na 30.3 wenye matatizo ya macho.

 

Nae Katibu wa Jumuiya ya Maradhi ya Kisukari Ali Zuber Juma alisema Jumuiya ya umoja wanaoishi na maradhi ya kisukari  iliosajiliwa Zanzibar Novemba 26,2006 kwa lengo la kuwainua wagonjwa wa maradhi ya kisukari.

 

Pia jumuiya hiyo inatoa elimu kwa walioathirika na maradhi yasioambukiza pamoja na jamii juu ya namna ya kujikinga na maradhi ya kisukari na kuwapa njia sahihi ya matumizi ya chakula ikiwemo mboga mboga na matunda

 

Kila ifikapo Novemba 14 ya kila mwaka ni siku ya Kisukari duniani ujumbe wa mwaka huu ni  Kauli mbiu ya mwaka huu ni “KISUKARI NA WAUGUZI

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.