Habari za Punde

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo akutana na watendaji sekta ya habari

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Khamis Abdala Said akizungumza machache nakumkaribisha Katibu mkuu kuhutubia katika mkutano wa katibu mkuu na wafanyakazi wa sekta ya Habari hafla iliyofanyika ukumbi wa sanaa Rahaleo Zanzibar.

Katibu Mkuu  Wizara ya Habari  Vijana Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab akiwahutubia Watendaji wa sekta ya habari (hawamo pichani) katika mkutano  uliyofanyika ukumbi wa sanaa Rahaleo Zanzibar.

Baadhi ya Wafanya kazi wa Sekta ya Habari wakifatilia hutuba ya katibu mkuu  wa  Wizara ya Habari  Vijana Utamaduni na Michezo (hayumo pichani) katika mkutano uliyofanyika  ukumbi wa sanaa Raha leo Zanzibar.

Mfanyakazi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Bahati Habibu akichangia mada  katika mkutano wa katibu Mkuu wa Wizara ya Habari  Vijana Utamaduni na Michezo na wafanyakazi wa Sekta ya habari katika     ukumbi wa sanaa Raha leo Zanzibar.

PICHA NA FAUZIA MUSSA /MAELEZO ZANZIBAR.

NA BAHATI HABIBU / MAELEZO       10/02/2021

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo amewataka wafanyakazi wa sekta ya habari kufanya kazi kwa ufanisi na mashirikiano ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Ameyasema hayo alipofanya ziara ya kujitambulisha na kuzungumza na wafanyakazi wa sekta ya hiyo huko ukumbi wa Sanaa uliopo Rahaleo mjini Zanzibar.

Amesema ili sekta hiyo ifanye kazi kwa ufanisi kila mfanyakazi atekeleze vyema majukumu yake kutokana na nafasi yake aliyopangiwa bila ya kujali changamoto zitakazojitokeza katika utendaji wa kazi zao.

Katibu huyo amewataka viongozi wa taasisi hizo kufanya usawa kwa wafanyakazi na kuacha tabia ya ubaguzi ili kuepuka mizozo na migogoro kwa kuwapatia stahiki zao bila ya upendeleo.

Aidha amewasisitiza wafanyakazi  kuwa na ushirikiano katika utendaji wa kazi zao na kuondoa makundi, ubaguzi na majungu ili kuweza kufanya kazi kwa kuleta maendeleo katika sekta hiyo.

“Ubaguzi, majungu na makundi katika utendaji wa kazi hurudisha nyuma utendaji wa kazi na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi ni vizuri kushirikiana na kupendana ili kuleta maendeleo ya nchi” alisema Katibu Mkuu.

Nae Naibu Katibu Mkuu Khamis Abdalla Said amesema atahakikisha kwamba anazitafutia ufumbuzi changamoto zote zinazowakabili wafanyakazi wa sekta ya habari ikiwa pamoja na kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

Hata hivyo amekemea matumizi mabaya ya fedha za umma kwa baadhi ya watendeji kutumia kwa maslahi yao binafsi au kwa wachache jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya taifa.

“Hatutakubali kuona fedha zilizochumwa kwa jasho la wanyonge zinatumika kwa maslahi ya watu wachache tutahakikisha kila fedha inayoingia inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa”, alisema Naibu Katibu.  

Akitoa neno la shukrani Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Omar Said ameiomba serikali kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa sekta ya Habari kutokana na mazingira magumu wanayokabiliana nayo ili kuweza kutoa huduma nzuri kwa jamii.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.