Habari za Punde

Mkutano wa Pili wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar waanza leo

Mwakilishi wa Kuteuliwa na Rais Nassor Ahmed Mazrui akisalimiana na Katibu Ngome ya Wanawake Taifa ACT-Wazalendo Janet Fussi wakati akiingia katika Ukumbi wa Baraza la kumi la Wawakilishi lililoanza leo Mbweni Zanzibar.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid pamojana makatibu wakiingia katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi ili kuanza mkutano wa  Pili wa Baraza la Kumi  lililoanza leo Mbweni Zanzibar.
 Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe,Zubeir Ali Maulid (kulia)akimuapisha Mhe ,Nassor Ahmed Mazrui kua Mjumbe wa Baraza hilo baada ya kuteuliwa na Rais Ndani ya Ukumbi wa  Baraza la Kumi  lililoanza leo Mbweni Zanzibar.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe,Zubeir Ali Maulid (kulia)akimuapisha Mhe ,Omar Said Shaaban kua Mjumbe wa Baraza hilo baada ya kuteuliwa na Rais Ndani ya Ukumbi wa  Baraza la Kumi  lililoanza leo Mbweni Zanzibar.
Baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika Mkutano wa  Pili wa Baraza la Kumi la Wawakilishi lililoanza leo Mbweni Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya  Makamu wa Pili wa Rais Sera Uratibu na Baraza la Wawakilishi Dkt,Khalid Salum Mohamed akijibu Maswali katika Mkutano  wa   Pili wa Baraza la Kumi la Wawakilishi  lililoanza leo Mbweni Zanzibar.

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mhe,Tabia Maulid Mwita akijibu Maswali katika Mkutano  wa   Pili wa Baraza la Kumi la Wawakilishi  lililoanza leo Mbweni Zanzibar.

PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.10-02-2021.

Na Mwashungi Tahir /Rahima Mohammed      10/2/2021

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema haitasita kutumia mfumo wa utoaji risiti kwa njia ya elektroniki bali kuufanyia marekebisho ili uwze kutumika kwa uhakika.

Akijibu suali la Mhe Machano Othman Said Muwakilishi wa Jimbo la Mfenesini alietaka kujua kuhusu changamoto ya ukusanyaji wa kodi kwa wafanya biashara huko katika Baraza la Wawakilishi Chukwani Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe Jamal Kassim Ali amesema katika kipindi cha majaribio mfumo huo ulibainika kuwa na dosari ambazo zimeanza kufanyiwa marekebisho.

 Amefahamisha kuwa mfumo huo wa majaribio umewashirikisha wafanya biashara 150 kutoka makundi tofauti ya biashara Unguja na Pemba.

Waziri Jamal amesema mfumo huo unatarajiwa kuanza kutumika mwezi wa April kwa watu wote waliosajiliwa kulipa kodi na kwamba hivi karibuni itazindua rasmin matumizi ya vifaaa vya mfumo wa kutolea risti za kieletroniki.

Aidha Waziri Jamali amewataka wananchi kudai risiti kila wanapolipa fedha kwa unuuzi wa mafuta ili kuimarisha maendeleo ya nchi na kufikia malengo yake.

Vilevile serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Mufti imekusudia kufanya uhakiki wa misikiti na madrasa zote za Zanzibar ili kuhakikisha misikiti na madrasa inasajiliwa kwa mujibu sheria na taratibu.

Akijibu suala la Mh Salma Mussa Bilali nafasi za wanawake alietaka kujua serikali imejipanga vipi kuhakisha misikiti na madrasa zote Zanzibar zinasajiliwa.

Waziri wa NchiOfisi ya Rais Katiba,Sheria Utumishi na Utwala bora Mhe Haroun Ali Suleiman amesema kwa sasa ofisi hiyo imeshaanza kufanya uhakiki wa madrasa za Mkoa wa Mjini Magharibi na Kaskazini Unguja ambapo zoezi hilo litaendelea Mkoa wa  Kusini Unguja na Mikoa yote ya Pemba.

Amesema ofisi hiyo imeeandaa utaratibu wa kufanya ukaguzi wa misikiti na madrasa ili kubaini matatizo yanayozikabili na kuyapatia ufumbuzi kwa kushirikiana na wananchi wenyewe.

Akiuliza suali la nyongeza  Mhe Panya Abdalla Nafasi za wanawake alilouliza kwanini walimu wa madrasa baadhi yao hawana taaluma ya kutosha na katika kusomesha na kutaka kujua ofisi hiyo imejipanga vipi.

Waziri Haroun amesema Ofisi ya Mufti imejipanga vzuri katika kuwapa elimu ili kupata walimu bora katika ufundishaji.

Akijibu suala la Mhe Abdallah Abas Wadi Jimbo la Nungwi kutokana na changamoto ya kukosekana kwa maji safi katika Kijiji cha Nungwi na Fukuchani Waziri wa Maji nishati  Suleiman Masoud Makame  amesema ZAWA inaendelea na zoezi hilo kwa kushirikiana na viongozi wa siasa wajimbo la Nungwi na Mkoa na wasamaria wema ili kuharakisha huduma hiyo ipatikane vyema.

Aidha kupitia Wizara ya Maji na Nishati imesema  ZAWA inaendelea na zoezi la kupitia mtandao wa maji kutoka katika vyanzo vitatu vinavyohudumia eneo la Nungwi  kwa kusawadhisha mivujo mingi inayotokana na hujuma za watu mbalimbali pamoja na kuondoa bomba zilizoharibika kwa lengo kuwafikia wananchi.

Wakati huohuo wajumbe wa Barza la Wakilishi wamewachagua wabunge watano  kuenda kushiriki katika Bunge la Jamuhuri ya MUUngano wa Tanzania ambao ni Ameir Abdallah Ameir,Mwantatu Mbarak Khamis,Bakari Hamadi Bakar,Suleimani Haroub Suleiman na Bahati Khamis Kombo.

Vilevile Baraza limechagua wenyeviti wa Baraza  Mwanasha Khamis Juma na Shabani Ali Othamani,pia limewachagua viongozi wa umoja wa wawakilishi  wanawake  ya Baraza la Wawakilishi (UWAWAZA)  ambapo Mwenyekiti Sada Mkuya Salum,Makamo mweyekiti  Mwantatu Mbaraka Khamis.

Aidha Anna Athanas Paul kuwa katibu wa umoja huo, mtunza hazina Panya Ali Abdallah pamoja na  wajumbe wakamati tendaji ya UWAWAZA Bahati Khamis Kombo,Salha Mohd Mwinjuma,Rukia Omar Mapuri na Mwanajuma Kassim Makame.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.