Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi
alifika nyumbani kwa kizuka wa Marehemu Seif Sharif Hamad huko Mbweni na
kuonana nae pamoja na familia yake na ya Marehemu huku akitumia fursa hiyo
kumuomba kizuka pamoja na wanafamilia kuwa na subira na Mwenyezi mungu atawafanyia
wepesi.
Akiwa huko nyumbani kwa Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad ambapo Mama Mariam Mwinyi na Alhaj Dk. Mwinyi, Rais Dk. Mwinyi alimuahidi kizuka huyo kwamba ataendelea kushirikiana nae wakati wote yeye pamoja na Serikali anayoiongoza.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment