Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Ameongoza Wananchi wa Zanzibar Katika Kuuaga Mwili wa Hayati Dkt.John Pombe Magufuli Uwanja wa Amaan Zanzibar.

GARI Maalum la JWTZ lililoandaliwa kwa ajili ya kubeba Mwili wa Hayati John Pombe Magufuli ukiwasili katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar, ukizungumka Uwanja baada ya kuwasili kwa ajili ya hafla ya kuaga kwa Wananchi wa Zanzibar.  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa amesimama na Viongozi wa jukwaa kuu wakati mwili wa Hayati John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ukiwasili katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar kwa ajili ya kuagwa na Wananchi wa Zanzibar. 
MAKAMANDA wa Jeshi la Wananchi Tanzania JWTZ wakiwa wamebeba jeneza likiwa na mwili wa hayati John Pombe Magufuli walipowasili Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa heshima za mwisho kwa Wananchi wa Zanzibar katika uwanja hivyo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa amesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa, katika hafla ya kuuaga mwili wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar, na (kulia kwa Rais) Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa na (kushoto kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
ASKARI wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakipiga saluti wakati ukipigwa wimbo wa Taifa katika hafla ya kumuaga Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar
ASKARI wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakipiga saluti wakati ukipigwa wimbo wa Taifa katika hafla ya kumuaga Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar

WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya mazishi Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi kuzungumza na Wananchi katika hafla ya kuuaga mwili wa Hayati Dkt.Jon Pombe Magufuli katika uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwahutubia Wananchi wa Zanzibar katika hafla ya kuuaga mwili wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania , hafla hiyo imefanyika katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar
WANANCHI wa Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia wakati wa hafla ya kuuaga mwili wa Hayati Dkt.John Pombe Magufuli, aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla hiyo imefanyika katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar
WANANCHI wa Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia wakati wa hafla ya kuuaga mwili wa Hayati Dkt.John Pombe Magufuli, aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla hiyo imefanyika katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akitowa heshima za mwisho kwa mwili wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa hafla ya kumuaga marehemu katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar leo 23/3/2021
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akitowa heshima za mwisho kwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla hiyo ya kumuaga imefanyika katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.