Habari za Punde

Tume ya UKIMWI Zanzibar Kukabiliana Vyema na Mazingira ya Sasa Kutumia Mbinu na Kuibua Mawazo Mapya Dhidi ya Maambukizi ya UKIMWI

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt.Omar Dadi Shajak akizungumza na Viongozi wa Tume ya Ukimwi Zanzibar, mazungumzo hayo yamefan yika katika ukumbi wa Ofisi ya Wizara hiyo Migombani Zanzibar.

Na.Raya Hamad.– OMKR  

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar D. Shajak ameitaka Tume ya UKIMWI Zanzibar kukabiliana vyema na mazingira ya sasa kwa kutumia mbinu na kuibua mawazo mapya ambayo yatazidisha mapambano dhidi ya maambukizi ya UKIMWI

Dkt Shajak ameyasema hayo alipofanya mazungumzo na viongozi pamoja na watendaji wa Tume ya UKIMWI ambapo amesisitiza kuwa jitihada zinazofanyika sasa katika kukabiliana na maambukizi ya UKIMWI yaende mbali zaidi kwa vile dunia hivi sasa nguvu kubwa imewekezwa kwenye kupambana na virusi vya Korona 

Amesema ugonjwa wa Korona umeipelekea jamii kujisahau kama ugonjwa wa UKIMWI bado upo hivyo Tume ya UKIMWI iendelee kuchukuwa nafasi yake katika kuelimisha jamii na kuhakikisha hakuna maambukizi mapya ya VIRUSI vya UKIMWI ifikapo 2025

“juhudi zetu zilenge mafanikio na kufikiria njia mbadala za kutatua matatizo yaliyopo, mpango mkakati wa nne ni vyema sasa ukaangalia mawazo mapya yatakayotuvusha hapa tulipo ili tuondokane na maradhi ya UKIMWI” alisisitiza

Nakueleza kuwa lengo la kupunguza na kuondokana na idadi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kawa mama kwenda kwa mtoto linafikiwa, Vijana na makundi maalum kufikiwa katika kupewa elimu, wenye mahitaji kupatiwa dawa na tiba sahihi

Nae Mkurugenzi mtendaji Tume ya UKIMWI Dkt Ahmeid M. Khatib amemuelezea Katibu Mkuu kuwa katika kufikia malengo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Tume inawajibu wa kutayarisha mkakati maalum na wadau wote wanajukumu la kuufuata mkakati huo

Tume ya UKIMWI inaendelea na matayarisho ya Mkakati wa nne wa UKIMWI utaogusa sekta zote kama taasisi za Serikali ama binafsi pamoja na jamii kwa vile wadau wote ni wa mapambano ya UKIMWI na hivyo ni wajibu wa kila anaeguzwa kuhakikisha malengo ya nchi na dunia yanafikiwa

Amesema mafanikio yaliyopatikana katika kudhibiti maradhi ya UKIMWI yamepelekea Zanzibar kufikia chini ya asilimia moja ya kiwango cha maambukizi ambapo nchi chache zimeweza kufikia malengo haya na kuifanya Zanzibar iwe ni moja kati ya nchi zenye mafaniko

Dkt Ahmeid amesema hadi kufikia mwaka 2020 malengo na shabaha za dunia ni kuhakikisha kuna 90 tatu ambazo zinafikiwa, na Zanzibar imefanikiwa kufikia asilimia 90 na amehakikisha asilimia 90 ya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI wanaojitambuwa ni asilimia 94, wanaojitambua na wanaotumia dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI ni asilimia 98 na wanaotumia dawa ambao wameweza kuvishusha virusi ndani ya mwili ni asilimia 93

Wakitoa maoni yao wafanyakazi wa Tume ya UKIMWI wameiomba  Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kutoa msukumo kwa Serikali kwa baadhi ya taasisi kuendelea kuunga mkono juhudi za mapambano ya maradhi ya UKIMWI kwani hakuna taasisi ambayo haijaguswa na changamoto ya maradhi ya UKIMWI

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais alieongozana na Mkurugenzi Mtendaji Tume ya UKUMWI na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa ZAYEDESA Mama Shadya Karume kisha kutembelea kituo rafiki wa vijana na huduma za afya kilichopo Miembeni pamoja na kutembela Kituo cha Programu ya shirikishi ya UKIMWI, homa ya ini, kifua kikuu na ukoma.

Aidha Dkt Shajak amezishukuru taasisi zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya UKIMWI na kuahidi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kupitia ZAC itaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja na wadau wote wa mapambano ya UKIMWI ili lengo lililowekwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar liweze kufikiwa

Lengo la ziara hio ni kuona yanayoendelea kwenye vituo hivyo, changamoto wanazokabiliana nazo na namna ya kuzitatua  ikiwa ZAC ndio mratibu wa masuala ya UKIMWI ili kujenga ufanisi katika kutoa huduma bora dhidi ya mapambano ya UKIMWI

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.