Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amesema kuwa, shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika (EAPCCO) litaendelea kuimarisha hali ya usalama kwenye nchi za shirikisho hilo kwa kufanya operesheni za pamoja na kuhakikisha wanadhibiti uhalifu unaovuka mipaka na kwa kubadilishana taarifa za uhalifu na wahalifu.
IGP Sirro amesema hayo
leo jijini Dar es salaam wakati alipokutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi wa nchi
ya DRC Congo, IGP Dieudonne Bahigwa ambaye amefanya ziara ya kikazi hapa nchini
ikiwa ni siku chache kabla ya kupokea kijiti cha Uwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu
wa Polisi Mashariki Mwa Afrika lenye jumla ya nchi 14 wananchama wa shirikisho
hilo.
No comments:
Post a Comment