Habari za Punde

Ubalozi Mdogo wa China Zanzibar Wakabidhi Vyarahani kwa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation.

 

BALOZI Mdogo wa China Anayefanyia Kazi zake Zanzibar Mhe. Balozi Zhang Zhzsheng akimkabidhi Vyarahani Afisa Mtendaji Mkuu wa Foundation ya Mama Mariam Mwinyi, “ Zanzibar Maisha Bora Foundation” Bi.Mwanaidi Mohammed Ali, akipokea kwa niaba ya Mwenyekiti wa Zanzibar Maisha Bora Foundation Mama Mariam Mwinyi,kwa ajili ya kusaidia kuwawezesha Wanawake, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ubalozi Mdogo wa China Mazizini Jijini Zanzibar leo 28-1-2022

Balozi wa China nchini Tanzania, Zhang Zhisheng amesema msaada wa Vyerahani uliotolewa na  Ubalozi huo kwa Jumuiya ya “Zanzibar Maisha Bora Foundation”, unalenga kuwawezesha wanawake wa Zanzibar ili kuondokana na umasikini.

Balozi Zhang amesema hayo wakati alipokabidhi  Vyerahani vinane kwa Uongozi wa  Jumuiya ya Zanzibar Maisha Bora Foundation,  hafla iliofanyika katika Ubalozi huo, uliopo  Mazizini Jijini Zanzibar.

Amesema msaada wa Vyerahani hivyo vinane, ni mwanzo wa misaada mbali mbali inayolengwa kutolewa na Ubalozi huo kwa Jumuiya hiyo ili  kuwawezesha wanawake wa Zanzibar kuinua maisha yao.

Nae, Mtendaji Mkuu wa Jumuiya hiyo Mwanaidi Mohamed Ali, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mama Mariam Mwinyi aliushukuru Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa msaada huo, na kusema hatua hiyo inaonyesha dhamira ya Ubalozi huo katika kushirikiana na Jumuiya hiyo, ili kuwawezesha wanawake  Zanzibar.

Alisema Jumuiya ya Zanzibar Maisha Bora Foundation inathamini msaada huo na itaendelea kushirikiana na Ubalozi huo, huku akiahidi kutumika vyema kwa malengo yaliokusudia.

Msaada wa Vyerahani vinane uliotolewa na Ubalozi wa China nchini Tanzania, unatokana na mkutano wa Wadau uliofanyika Januari 26, mwaka katika Hoteli ya Golden Tulip,  Zanzibar – Airport, uliolenga kuwahamaisha wadau mbali mbali kushirikiana na Jumuiya hiyo ili kufanikisha malengo yaliokusudiwa.

Jumuiya ya Zanzibar Maisha Bora Foundation, ambapo malengo yake makuu ni kuinua maisha ya wanakake wa Zanzibar kuondokana na umasikini, inatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi ujao.

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,

Ikulu Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.