Habari za Punde

Maafisa habari watakiwa kuwapatia taarifa wananchi

Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Zanzibar  Dkt.Hassan Khatib Hassan akizungumza machache na kumkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Habrai ,vijana , utamaduni na Michezo ndugu Fatma Hamad Rajab kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Mh. Tabia Maulid Mwita  kuwahutubia maafisa habari  na mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika mkutano ulioandaliwa na Idara ya Habari Maelezo huko Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul-Wakil Kikwajuni Zanzibar.
Baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakifuatilia  hotuba ya Waziri wa Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Mh.  Tabia Maulid Mwita, iliyosomwa na Katibu  Mkuu wa Wizara hiyo (hayumo pichani) ndugu Fatma Hamad Rajab katika mkutano ulioandaliwa na Idara ya Habari Maelezo huko Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul-Wakil Kikwajuni Zanzibar.


Katibu  Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Ndugu  Fatma Hamad Rajab akihutubia katika mkutano wa Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo  Mh.Tabia Maulid Mwita huko Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul-Wakil Kikwajuni Zanzibar.
Afisa Habari Mkuu  Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Ndugu Raya Hamadi akitoa neno lelo shukurani kwaniaba ya Maafisa Habrai na Mawsiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Mkutano wa Maafisa hao uliandaliwa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar huko Ukumbi wa Sheikh Idrisa Badul-wakil Kikwajuni.

Afisa Habari kutoka mfuko wa  Hifadhi ya Jamii (ZSSF) Mussa Yussuf akizungumza katika mkutano wa Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar huko Ukumbiwa Sheikh Idrisa Badul-wakil Kikwajuni.

PICHA NA FAUZIA MUSSA- MAELEZO ZANZIBAR.


Na Mwashungi Tahir           Maelezo  

Maafisa Habari nchini wametakiwa kutumia ujuzi walionao ili kuwapatia taarifa wananchi juu ya utekelezaji wa mipango ya serikali, mafanikio pamoja na changamoto zake. 

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya habari, vijana,utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab kwa niaba ya Waziri wa habari wakati alipokuwa akizungumza katika mkutano wa Maafisa wa Habari na mawasiliano wa Serikali huko Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil, Kikwajuni.

Amesema ana matarajio makubwa baada ya mkutano huo kuwa, utoaji wa taarifa juu ya shughuli za serikali ya awamu ya nane utaimarika ili kila mwananchi ajue yanayofanywa na serikali.

Katibu huyo amesema Rais wa Zanzibar Dk. Mwinyi amekuwa akihimiza kila siku wananchi kupatiwa taarifa zinazofanywa na Serikali kutokana na umuhimu wa habari katika maendeleo ya nchi.

Kutokana na hali hiyo Katibu huyo amesema kwa Wizara yake kupitia Idara ya habari Maelezo itafanya uhakiki wa maafisa hao jinsi wanavyofanya kazi katika taasisi zao.

Amefahamisha kuwa Afisa husika atakaeshindwa kutekeleza vyema majukumu yake bila ya kujali taasisi anayofanyia kazi Wizara ya habari itapendekeza kwa Idara ya Utumishi kupatiwa kazi nyengine.

“Kuanzia sasa tutaendelea kuwafuatilia Maafisa habari wote kuhusu utendaji kazi zao, afisa yeyote atakayeshindwa kutekeleza vyema majuku tutaiomba Utumishi impatie kazi nyingine” Alisema Katibu huyo kwa niaba ya Waziri.

Awali akimkaribisha mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Habari Maelezo Zanzibar Hassan Khatib amesema tayari Wizara kupitia Idara ya Habari Maelezo imeshakamilisha muundo wa Utumishi wa Kada ambapo baada ya kuupitia utawasilishwa utumishi kwa ajili ya hatua muafaka.

Amesema Serikali imeamua kuitambua rasmin kada ya habari na mawasiliano ambapo muongozo umetolewa kwa Idara ya Habari Maelezo kuwaratibu maafisa wa habari na mawasiliano wote wa Serikali ili kuwatambua na kuwafanyia tathmini ya utendaji wao.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.