Habari za Punde

Kikao cha Kamati Tendaji ya chama cha Wanasheria wa Mabunge ya Afrika kuanza leo

  Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar 

Rais wa Chama cha Wanasheria wa Mabunge ya Afrika,  Mussa Kombo Bakar amesema dhana mpya ya ufuatiliaji wa sheria inatarajiwa kufanyiwa kazi ili kuhakikisha sheria zinazopitishwa zinatekelezwa ipasavyo.


Amesema  suala la kufuatilia sheria ni moja ya jambo la msingi  la kuhakikisha sheria zinaz otungwa zinatekelezwa .


Hayo ameyasema katika ukumbi wa Baraza la wawakilishi  Chukwani  wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu kikao cha siku mbili cha Kamati Tendaji  ya chama cha Wanasheria wa Mabunge ya  Afrika ambacho kinatarajiwa kufanyika leo hapa Zanzibar.


Aidha alisema kumekuwa na udhaifu wa utekelezaji wa sheria kwamba sheria nyingi zinazotungwa hazifanyiwi kazi .


Alifahamisha kuwa lengo la Mkutano wa kamati hiyo ni kufanya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanasheria wote wa Mabunge ya Afrika ambao unatarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu .


Alifahamisha  kuwa azma ya kuundwa chama hichi ni kubadilishana uzoefu pamoja na  kuongeza ujuzi miongoni mwa Wanasheria wa Mabunge  mbali mbali ya afrika


Chama cha Wanasheria wa Mabunge ya Afrika kimeanzIishwa mwaka 2011  nchini Nairobi Kenya ambacho kimekusanya Wanasheria wa Mabunge mbali mbali wa afrika.   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.